•Siku ya Jumatatu Manchester walifunga uwanja wa Carrington kufuatia visa vya Covid 19 vilivyoripotiwa kwenye kambi lao
Mechi kati ya Machester united na Brentford imeahirishwa kufuatia kusambaa kwa Corona kwenye kambi la manchester united.
Kupitia mtandao wa Twitter Manchester united wamesema ligi kuu ya Uingereza imekubali kusitisha mechi yao na Brentford iliyotarajiwa kuchezwa usiku wa Jumanne kati yao na Bentford.
Siku ya Jumatatu Manchester walifunga uwanja wa Carrington kufuatia visa vya Covid 19 vilivyoripotiwa kwenye kambi lao. Hii ni baada ya wafanyakazi kadhaa kupimwa na kupatikana na virusi hivo.
Kufuatia hayo klabu iliwandikia EPL barua ikieleza jinsi hali ilivyo katika uwanja wao.
EPL ilikubali ombi lao na kuahirisha mechi hadi wakati usiodhibitishwa.
Hivi karibuni visa vya Corona vimeripotiwa kuongezeka katika nchi ya Uingereza na kusababisha kuahirishwa kwa mechi kadhaa.
Timu ambazo zimeadhiriwa zaidi na virusi hivo ni Tottenham, Brighton na hivi karibuni machester imetangaza kuadhiriwa pia.
Hofu kubwa kwaa sasa ni kwamba kufuaitia yanayojiri huenda EPL ikapiga marufuku mashabiki kuhudhuria mechi zitakazochezwa siku zijazo.