logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Man United wanatarajia kukamilisha dili la kumnunua kipa wa Inter Milan, Andre Onana

Manchester United wana matumaini ya kukamilisha dili la kumnunua kipa wa Inter Milan Andre Onana.

image
na SAMUEL MAINA

Michezo08 July 2023 - 05:03

Muhtasari


  • •Mkufunzi wa United Erik ten Hag ana nia ya kusuluhisha wasiwasi kuhusu hali ya walinda mlango Old Trafford.
  • •Hag alimfundisha Onana katika Ajax na Mholanzi huyo anaamini kuwa mchezaji huyo yuko katika kiwango anachohitaji .

Manchester United wana matumaini ya kukamilisha dili la kumnunua kipa wa Inter Milan Andre Onana.

Mkufunzi wa United Erik ten Hag ana nia ya kusuluhisha wasiwasi kuhusu hali ya walinda mlango Old Trafford huku kukiwa na sintofahamu juu ya mustakabali wa David de Gea.

Mkataba wa De Gea huko Old Trafford ulimalizika mwishoni mwa mwezi uliopita bila makubaliano kuhusu ofa iliyopitiwa tena aliyopewa mchezaji huyo wa zamani wa kimataifa wa Uhispania.

Onana, 27, alicheza pasi nane katika mechi 24 kwenye Serie A msimu uliopita.

Mcameroon huyo pia alipeana pasi nane bila mabao katika mechi 13 za Ligi ya Mabingwa msimu uliopita - nyingi zaidi ya golikipa yeyote katika shindano hilo.

Hag alimfundisha Onana katika klabu ya zamani ya Ajax na Mholanzi huyo anaamini kuwa mchezaji huyo yuko katika kiwango anachohitaji na atazoea maisha ya Ligi Kuu kwa urahisi.

Kinyume chake, Ten Hag haamini kwamba uwezo wa De Gea akiwa na mpira miguuni mwake uko kwenye kiwango kinachohitajika.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved