Aliyekuwa kocha wa Tusker na Sofapaka Sam Timbe amefariki dunia.
Habari kuhusu kifo cha kocha huyo mkongwe zilitangazwa na URA FC ya Ligi Kuu ya Uganda Jumamosi, Agosti 19, 2023.
“Tunasikitika kuwataarifu msiba wa mheshimiwa kocha wetu mkuu, Sam Timbe, mchana wa leo akiwa njiani kupelekwa Hospitali ya Nakasero kwa ICU, kama alivyopewa rufaa na Hospitali ya St.
“Mawazo yetu yapo kwa familia yake na wapenzi wake katika kipindi hiki kigumu, kwa sasa timu yetu iko kambini katika hoteli ya Standard, Kampala, kujiandaa na mchezo ujao wa nusu fainali ya Kombe la FUFA Super 8 dhidi ya KCCA FC, unaotarajiwa kuchezwa keshokutwa [Jumapili. ] kwenye Uwanja wa MTN Omondi.
"Sasisho zaidi zitatolewa kwa wakati ufaao," URA ilitangaza.
Klabu hiyo ya Uganda ilikumbwa na taarifa za kifo cha Timbe walipokuwa kambini wakijiandaa kwa fainali ya Kombe la FUFA Super 8 dhidi ya KCCA FC iliyopangwa Jumapili kwenye Uwanja wa Philip Omondi mjini Kampala.
Timbe alijiunga na Tusker Januari 2018 baada ya klabu hiyo kuachana na Mganda mwingine George 'Best' Nsimbe.
Hata hivyo alikaa kwa muda mfupi kwani alitimuliwa baada ya mechi 11 pekee kufuatia msururu wa matokeo duni.
Mpaka kifo chake, Timbe alikuwa na miaka 69.