logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Alikiba kutumbuiza kwenye sherehe za ufunguzi wa African Football League

Mataifa 8 ya Afrika yalipata nafasi murwa ya kutoa timu 8 ambazo zitashiriki kwenye kinyang’anyiro hicho.

image
na Davis Ojiambo

Michezo20 October 2023 - 06:05

Muhtasari


  • • Mechi ya ufunguzi itakuwa kati ya Simba SC wakiwa kama mwenyewe wa mashindano hayo dhidi ya Al Ahly kutoka Misri.
  • • Shindano hilo la kipekee lilizinduliwa mwaka jana likiwa na dau ya zawadi la dola milioni 4 kwa washindi.
Alikiba kutumbuiza AFL

Msanii wa kizazi kipya wa muda mrefu kutokea nchini Tanzania, Alikiba amethibitisha kuwa atakuwepo kama mmoja wa wasanii watakaotumbuiza kwenye sherehe za ufunguzi wa shindano la African Football League.

Shindano hilo linazinduliwa leo Ijumaa, Oktoba 20 katika uwanja wa kimataifa wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam nchini Tanzania na linajumuisha vilabu wa mpira pendwa wa miguu kutoka mataifa 8 kote Afrika.

Ikiwa ni siku ya kwanza kwa mashindano hayo, kama kawaida kutakuwepo na sherehe za ufunguzi ambazo Alikiba kupitia ukurasa wake wa X, awali ukijulikana kama Twitter amethibitisha kutia nakshi kwenye nyuso za mashabiki wake.

“Sherehe za Kufungua ligi ya mpira wa miguu Afrika… Tukutane Ijumaa kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa,” Alikiba aliandika mapema Alhamisi huku akipakia picha za mara ya mwisho akitumbuiza katika uwanja huo mwezi Agosti wakati wa Simba Day – siku ya klabu ya Simba SC kusherehekea ufunguzi wa msimu mpya na mashabiki wake.

Mataifa 8 ya Afrika yalipata nafasi murwa ya kutoa timu 8 ambazo zitashiriki kwenye kinyang’anyiro hicho.

Timu hizo 8 zitakuwa ni Simba SC kutoka taifa la Tanzania, Mamelodi Sundowns kutoka Afrika Kusini, Petro Atletico de Luanda kutoka Angola, TP Mazembe ya DRC, Esperance ya Tunisia, Al Ahly ya Misri, Enyimba ya Nigeria na Wydad ya Morocco.

Mechi ya ufunguzi itakuwa kati ya Simba SC wakiwa kama mwenyewe wa mashindano hayo dhidi ya Al Ahly kutoka Misri.

Shindano hilo la kipekee lilizinduliwa mwaka jana likiwa na dau ya zawadi la dola milioni 4 kwa washindi.

Taarifa amabzo hata hivyo hazijathibitishwa zinaakisi kwamba rais wa FIFA Gianni Infantino na aliyekuwa mkufunzi wa muda mrefu wa Arsenal ya Uingereza, Arsene Wengr ni miongoni mwa majina makubwa watakaoshuhudia ufunguzi wa kinyang’anyiro hicho.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved