DR Congo ilitinga hatua ya mtoano ya Kombe la Mataifa ya Afrika 2023 baada ya kutoka sare tasa na Tanzania mjini Korhogo.
Matokeo hayo yaliwaondoa Waafrika hao wa Mashariki, ambao walihitaji kushinda ili kuendelea.
Pointi moja ilitosha kwa DR Congo kumaliza nafasi ya pili katika Kundi F nyuma ya Morocco, walioongoza jedwali kutokana na ushindi wao wa 1-0 dhidi ya Zambia.
Zawadi ya Leopards ni hatua ya 16 bora dhidi ya Misri, huku Morocco ikimenyana na Afrika Kusini.
Matokeo ya Kundi F pia yalitosha kuwaona wenyeji wa michuano hiyo Ivory Coast wakipenya hadi katika raundi ya pili kama timu nne bora zilizoshika nafasi ya tatu.
The Elephants - ambao walikuwa wamemfuta kazi bosi Jean-Louis Gasset mapema Jumatano baada ya kumaliza wa tatu katika Kundi A - watamenyana na mabingwa watetezi Senegal katika hatua ya 16 bora Jumatatu.
Leopards walikuwa bora katika mchuano huo
Katika mechi ngumu ambapo timu zote zilikosa nafasi za wazi, hakuna timu iliofanikiwa kuinggia katika lango la mwengine na kjufunga goli
Wakichochewa na wafuasi wengi wenye sauti na uchangamfu ambao walizidi sauti za wafuasi wa, DR Congo ilitengeneza fursa bora zaidi katika kipindi cha ufunguzi.
Gael Kakuta alipiga mpira wa adhabu uliokamatwa moja kwa moja na kipa wa Taifa Stars, Aishi Manula, ambaye pia alitoka nje kwa kasi na kuzuia shambulio la Fiston Mayele kwenye eneo la hatari.
Pasi nzuri ya Kakuta kwa Yoane Wissa pia iliokolewa na kipa huyo aliposalia na mshambuliaji huyo wa Brentford
Meschack Elia wa DR Congo akijibu hoja wakati wa mchezo wao wa Kombe la Mataifa ya Afrika 2023 dhidi ya Tanzania
Nahodha wa Tanzania Mbwana Samatta alijitahidi sana katika timu yake akilizunguka eneo la hatari na kupiga shuti kali kutoka pembeni.
Nafasi zilikuwa nyingi zaidi katika kipindi cha pili hadi Wissa alipotengeneza nafasi mbili hatari katika kipindi cha mwisho cha mchezo.
Kwanza, Manula aliokoa shambulio zuri kutoka kwa mchezaji huyo wa Brentford baada ya kujinyoosha ili kupangua mpira uliotarajiwa kuchezesha wavu.
Lakini ukweli, ukungu mwepesi uliposhuka kwenye Uwanja wa Amadou Gon Coulibaly, hakuna upande ulioonekana kama kutafuta njia ya kupata bao.
Matokeo hayo yanamaanisha Tanzania iliandikisha sare tasa kwa mara ya kwanza katika Kombe la Mataifa ya Afrika, na kwamba bado hawajashinda katika mechi tisa za michuano hiyo, wakimaliza mkiani mwa kundi lao kwa mara nyingine.
Washindi mara mbili DR Congo wametinga hatua ya mtoano kwa mara ya tano katika mechi sita zilizopita kwenye fainali na watafurahia nafasi yao ya kushinda timu ya Misri itakayomkosa Mohamed Salah wakati timu hizo mbili zitakapokutana San Pedro Jumapili (20:00). GMT).