logo

NOW ON AIR

Listen in Live

UEFA kuchunguza Demiral kufuatia ishara marufuku ya kusherehekea

Beki huyo alisherehekea bao lake la pili kwa ‘wolf salute’, ishara iliyo marufuku Ufaransa na Austria

image
na Davis Ojiambo

Michezo04 July 2024 - 05:09

Muhtasari


  • •Alisherehekea bao lake la pili kwa ‘wolf salute’, ishara inayohusishwa na kundi la itikadi kali za mrengo wa kulia la Gray Wolves ambalo linahusishwa na chama tawala cha Uturuki 
  • •"Ninajivunia sana kwa sababu mimi ni Mturuki, kwa hivyo baada ya bao nilihisi mshawasha sana na nilitaka kusherehekea hivyo, na nina furaha sana kuifanya." Alisema beki huyo.

Beki wa Uturuki Merih Demiral anachunguzwa na Uefa baada ya kuonekana kusherekea kwa utovu wa nidhamu kufuatia ushindi wa nchi yake dhidi ya Austria.

Demiral, 26, alifungia mara mbili Uturuki ambapo ilijikatia tiketi ya robo fainali ya Euro 2024 kumenyana na Uholanzi baada ya kushinda 2-1 dhidi ya Austria.

Beki huyo wa Al-Ahli alisherehekea bao lake la pili kwa ‘wolf salute’, ishara inayohusishwa na kundi la itikadi kali za mrengo wa kulia la Gray Wolves ambalo linahusishwa na chama tawala cha Uturuki cha National Movement Party.

Demiral alisema salamu hiyo, ambayo imepigwa marufuku nchini Austria na Ufaransa, ilipangwa mapema iwapo angefunga.

"Nilikuwa na lengo kusheherehekea hivyo akilini baada ya kufunga," Demiral alisema.

"Ninajivunia sana kwa sababu mimi ni Mturuki, kwa hivyo baada ya bao nilihisi mshawasha sana na nilitaka kusherehekea hivyo, na nina furaha sana kuifanya." Alisema beki huyo.

Demiral alichapisha picha ya kusherehekea huko kwenye akaunti yake ya X na nukuu: "Ni furaha iliyoje yule anayesema mimi ni Mturuki!"

kwenye akaunti yake ya X na nukuu: "Ni furaha iliyoje yule anayesema mimi ni Mturuki!"

Uchunguzi wa Uefa umefunguliwa kwa mujibu wa Kifungu cha 31(4) kuhusiana na "tabia isiyofaa inayodaiwa" ya Demiral.

Iwapo atapatikana na hatia, Demiral anaweza kutozwa faini au kufungiwa asicheze huku Uturuki ikijiandaa kumenyana na Uholanzi katika robo fainali Jumamosi.

Kiungo wa kati wa Uingereza Jude Bellingham anachunguzwa kwa ishara aliyoifanya wakati wa ushindi wa hatua ya 16 bora dhidi ya Slovakia siku ya Jumapili.

Bellingham alionekana akifanya ishara ya kukaba kuelekea benchi ya Slovakia baada ya kufunga mkwaju wa juu katika dakika za lala salama.

Uchunguzi wa Uefa umefunguliwa kwa mujibu wa Kifungu cha 31(4) kuhusiana na "tabia isiyofaa inayodaiwa" ya Demiral.

Iwapo atapatikana na hatia, Demiral anaweza kutozwa faini au kufungiwa asicheze huku Uturuki ikijiandaa kumenyana na Uholanzi katika robo fainali Jumamosi.

Kiungo wa kati wa Uingereza Jude Bellingham anachunguzwa kwa ishara aliyoifanya wakati wa ushindi wa hatua ya 16 bora dhidi ya Slovakia siku ya Jumapili.

Bellingham alionekana akifanya ishara ya kukaba kuelekea benchi ya Slovakia baada ya kufunga mkwaju wa juu katika dakika za lala salama.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved