Afisa wa serikali Argentina afutwa kazi kwa kumtaka Messi aombe msamaha

Julio Garro alifutwa kazi baada ya baada ya kudai kuombwa msamaha na nyota wa soka Lionel Messi.

Muhtasari

•Utata ulizuka baada ya video kuibuka ikionyesha wachezaji wakiwacheka wachezaji wa soka wa Kifaransa wenye asili ya Kiafrika.\

•Hata hivyo, matamshi yake yalijibiwa haraka na majibu makali kutoka kwa serikali ya Argentina.

Lionel Messi
Image: INSTAGRAM

Afisa wa Argentina amepigwa kalamu baada ya kumkosoa nahodha wa timu ya taifa ya soka, Lionel Messi.

Julio Garro, Naibu Katibu Mkuu wa Michezo wa Argentina, alifutwa kazi baada ya baada ya kudai kuombwa  msamaha na nyota wa soka Lionel Messi.

Tukio hilo linahusiana na nyimbo zinazodaiwa kuwa za ubaguzi wa rangi zilizotungwa na wachezaji wa timu ya soka ya Argentina wakati wa sherehe za ushindi wao wa Copa America dhidi ya Colombia.

Utata ulizuka baada ya video kuibuka ikionyesha wachezaji wakiwatania wachezaji wa soka wa Kifaransa wenye asili ya Kiafrika.

Moja ya mistari katika wimbo huo uliokuwa na utata ilirejelea urithi wa Kiafrika wa wachezaji wa Kifaransa, jambo lililosababisha hasira na kukashifiwa ulimwenguni kote, ikiwa ni pamoja na na Shirikisho la Soka la Ufaransa (FFF).

Garro, kujibu video hiyo kuwa maarufu, alitoa wito kwa Lionel Messi na Claudio Fabian Tapia, Rais wa Shirikisho la Soka la Argentina, kutoa maombi ya msamaha.

Aliibua wasiwasi kuwa tabia kama hizo zinachafua sifa ya Argentina kimataifa. "Nadhani Messi anapaswa kuomba msamaha wa kutosha kwa niaba ya timu, vilevile Rais wa Shirikisho la Soka la Argentina," Garro alisema katika mahojiano ya redio.

Hata hivyo, matamshi yake yalijibiwa haraka na majibu makali kutoka kwa serikali ya Argentina.

Ofisi ya Rais Javier Milei ilitangaza kufutwa kazi kwa Garro, ikisema kuwa "hakuna serikali inayoweza kudai maoni au hatua zinazochukuliwa na Timu ya Taifa ya Argentina au raia yeyote."

Uamuzi wa kuondoa Garro kutoka kwa nafasi yake kama Naibu Katibu Mkuu wa Michezo ulionyesha msimamo wa serikali kuhusu uhuru wa kujieleza na utaalamu wa taasisi za michezo.

Wakati huo huo, FIFA imeanzisha uchunguzi kuhusu tukio hilo, ikilaani aina yoyote ya ubaguzi ikiwemo ubaguzi wa rangi.

Shirikisho hilo la soka ulimwenguni lilisisitiza azma yake ya kupambana na ubaguzi wa aina zote, ikiwa ni pamoja na wachezaji, mashabiki, na maafisa.