“Nilipatwa na trauma nikiwa Arsenal, waliniita flop namba 1 katika historia ya EPL!” – Nicolas Pépe

Mshika Bunduki huyo wa zamani alifichua kuwa "nilikuwa na chuki na soka. Nilipoacha kucheza, nilijiuliza kwa nini nilikuwa kwenye fani hii. Nilikuwa na mashaka mengi sana hivi kwamba nilifikiria kuacha.”

Muhtasari

• Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ivory Coast ametafakari safari yake na The Gunners katika mahojiano na jarida la Ufaransa, L’Equipe.

• Alipowasili kwa ada kubwa ya €80M, uhamisho uliovunja rekodi kwa Arsenal, Nicolas Pépé alishindwa kukidhi matarajio yaliyowekwa ndani yake.

NICOLAS PEPE
NICOLAS PEPE
Image: x

Mwaka mmoja baada ya kuondoka Arsenal, mchezaji wa Ivory Coast, Nicolas Pépé (29) ni mchezaji huru kufuatia mkataba wake kumalizika Trabzonspor.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ivory Coast ametafakari safari yake na The Gunners katika mahojiano na jarida la Ufaransa, L’Equipe.

Alipowasili kwa ada kubwa ya €80M, uhamisho uliovunja rekodi kwa Arsenal, Nicolas Pépé alishindwa kukidhi matarajio yaliyowekwa ndani yake.

Katika mechi 112 akiwa na The Gunners, winga huyo alifunga mabao 27 na asisti 21 kabla ya kujiunga na Uturuki msimu uliopita wakati Trabzonspor ilipompa mkataba wa mwaka mmoja.

Huko, alifanikiwa kupata ujasiri, akifanikiwa kupata matokeo mazuri kwenye hatua ya kitaifa na kimataifa, akimaliza wa tatu kwenye ligi kuu ya Uturuki, akishinda AFCON na Ivory Coast.

Njia ya kurudisha mapenzi yake kwa mchezo baada ya safari ngumu huko Arsenal.

Katika mahojiano na L’Equipe, Nicolas Pépé alifichua kwamba “alikuwa amepatwa na aina fulani ya kiwewe, kana kwamba niliporwa mapenzi yangu.”

Mshika Bunduki huyo wa zamani alifichua kuwa "nilikuwa na chuki na soka. Nilipoacha kucheza, nilijiuliza kwa nini nilikuwa kwenye fani hii. Nilikuwa na mashaka mengi sana hivi kwamba nilifikiria kuacha.”

“Nilijiuliza ni kwa jinsi gani wangeweza kuwa wagumu sana kwangu. Walifikia hatua ya kuniita flop mkubwa zaidi katika historia ya Ligi Kuu! Lakini nilikataa kusugua kiti.”