logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Rashford Azungumza Baada Ya Kukamilisha Uhamisho Kwenda Aston Villa

Rashford alikamilisha uhamisho kutoka Man United kwenda Aston Villa Jumapili jioni.

image
na Samuel Mainajournalist

Football03 February 2025 - 07:05

Muhtasari


  • Rashford ataichezea Villa kwa muda uliosalia wa msimu wa 2024/25 na klabu hiyo itagharamia 75% ya mshahara wake wakati huo.
  • Villa watakuwa na chaguo la kumnunua kabisa kwa pauni milioni 40 baada ya kumalizika kwa muda wa mkopo mwezi Juni.


Mchezaji wa Kimataifa wa Uingereza Marcus Rashford alikamilisha uhamisho kutoka Manchester United kwenda Aston Villa Jumapili jioni.

Villa ilithibitisha kumsajili winga huyo mwenye umri wa miaka 27 kwa mkopo kupitia kurasa zao rasmi za mitandao ya kijamii.

"Aston Villa ina furaha kutangaza kumsajili kwa mkopo Marcus Rashford kutoka Manchester United," Villa ilisema katika taarifa kwenye X.

Rashford anaripotiwa kufanyiwa uchunguzi wa kimatibabu katika Villa Park siku ya Jumapili kabla ya kujiunga na kikosi hicho kinachonolewa na Unai Emery.

Mshambulizi huyo ataichezea Villa kwa muda uliosalia wa msimu wa 2024/25 na klabu hiyo yenye maskani yake Birmingham itagharamia 75% ya mshahara wake wakati huo. Kwa kawaida anapokea mshahara wa Pauni 325,000 kwa wiki katika Man United.

Villa walikabiliwa na ushindani mkubwa kutoka kwa vilabu vingine kupata saini ya winga huyo mwenye umri wa miaka 27 na watakuwa na chaguo la kumnunua kabisa kwa pauni milioni 40 baada ya kumalizika kwa muda wa mkopo mwezi Juni.

"Ningependa kuwashukuru Manchester United na Aston Villa kwa kufanikisha mpango huu wa mkopo," Rashford alisema baada ya kukamilisha uhamisho huo.

"Nilikuwa na bahati kuwa na vilabu vichache vilivyonikaribia lakini Aston Villa ulikuwa uamuzi rahisi kufanya- nafurahia sana jinsi Aston Villa imekuwa ikicheza msimu huu, na matarajio ya wasimamizi," aliongeza.

Pia alieleza kuhusu kiasi gani anataka kucheza tena baada ya kuwekwa nje na kocha wa Man United, Ruben Amorim katika wiki kadhaa zilizopita.

"Nawatakia kila la heri Manchester United kwa kipindi kizima kilichosalia," alisema.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved