Tangia wakati huo serikali na idara mbali mbali za usalama wa majini wakiwemo wapiga mbizi wa kibinafsi wamekuwa wakiendelea na juhudi za kuiondoa miili hiyo pamoja na gari hilo bila mafanikio .Siku ya jumatano msemaji wa serikali Cyrus Oguna kwa mara ya kwanza alitoa matumaini kwa familia na wakenya kwa kutangaza kwamba kifaa kinachofanana na gari kilionekana umbali wa mita zaidi ya 50 chini ya bahari na kutoa fursa ya oparesheni ya leo kuliondoa gari hilo .
John Wambua ,mume wa marehemu Miriam Kighenda na ambaye pia alimppteza binti yake Amanda Mutheu katika mkasa wa Likoni
Gari hilo lilivutwa kwa kreni katika oparesheni iliyochukua saa nane na kufikia saa kumi na dakika 12 ijumaa ,gari lenyewe liliondolewa na kuwekwa ardhini . Mumewe Miriam ,John Wambua alikuwa katika eneo la mkasa wakati gari gilo lilipokuwa likivutwa kutoka baharini .Umati wa watu ulijaa katika fuo za bahari kujionea oparesheni hiyo licha ya polisi kuwaondoa mamia ya wananchi waliokuwa na hamu ya kushuhudia shughuli ya kuondoa gari hilo .