Seli ya mahaba:Mimi na baba mtoto wa Maribe ni marafiki-Ujumbe wa Itumbi kwa Eric Omondi

Dennis Itumbi kwa mara ya kwanza amezungumzia uhusiano wake na babake mtoto wa rafikiye Jacque Maribe, alisema kuwa ni marafiki wakiwa na mcheshi Eric Omondi.

Akiongea jana usiku katika uzinduzi wa klabu cha mcheshi chipukeezy alisema ni marafiki wa dhati wakiwa wawili.

"Sisi ni marafiki wakaribu na wazuri sana,uwa namsaidia katika biashara zake kwa mara nyingi na pia yeye uwa ananisaidia katika biashara zangu ndogo

Nikifungua mkahawa uwa anakuja na kufanya onyesho lake katika eneo hilo, kama ana mahali anaenda kufanya biashara zake uwa nampa msaada anaohitaji." Aliongea Itumbi.

Itumbi na mwanahabari Jacque Maribe ni marafiki wa dhati ambaye pamoja mcheshi Erick Omondi wana mtoto kwa jina Zahara.

Hapo awali mashabiki wa Jaque na Eric walidhani wawili hao wanachumbiana,walijuwa ukweli wakati wazazi hao walipotundika  picha katika mtandao wao wa kijamii wakiwa na mtoto wao.

"Family first.happy graduation day Zahari. we mum and dad@EricOmondi are proud of you." Jacque Aliandika.

Kwa hivo sasa mnafahamu vyema wanaume hao wawili wamesimama wapi katika maisha ya Jacque.