Huu ni mkutano wa pili Rais Kenyatta ameandaa na viongozi hao wa mlima Kenya baada ya kuchaguliwa kuhudumu katika muhula wake wa pili.
Hisia mbali mbali zimezidi kuibuka kuhusiana na mkutano huo kwani chama cha Jubilee ambacho kwa sasa kimedaiwa kugawanyika kwa vipande viwili, upande wa tanga tanga na mrengo wa kieleweke, wote watahudhuria mkutano huo.
Tanga tanga kwa upande mwingine wameonekana kumpigia debe naibu wa Rais William Ruto, wakisisitiza kuwa Naibu huyo atawania kiti cha urais mwaka wa 2022, baada ya Rais Kenyatta kumaliza muhula wake.
Mrengo huo wa tanga tanga unaongozwa na mbunge wa Kikuyu Kimani Ichung'wa na mbunge wa Kiharu Ndindi Nyoro na baadhi ya wengineyo.
Suala kubwa likibakia je, Rais Kenyatta ataweza kuleta umoja katika chama hicho cha Jubilee?