Iliripotiwa kwamba Raburu na mkewe walikuwa wameachana na kila mmoja kuishi katika nyumba yake baada ya mtangazaji huyo wa 10 over 10 kuwa na uhusiano wa pembeni.
Katika madai hayo, iliwekwa picha ya kipusa mmoja mrembo kupindukia ambaye alidaiwa kuwa sasa ndiye anampa joto la usiku Raburu. Hata hivyo, inafichuka kwamba mrembo huyo ni mwathiriwa wa utumizi wa mitandao bila uthibitishaji wa maelezo na picha kwani hata hamjui Raburu. Jina lake limetambuliwa katika instagram kama Miva Noelle.
Sasa inabainika kwamba msichana huyo ni Mnyarwanda na sio Mganda kama ilivyokuwa ikidawa katika mitandao hapo awali
Picha za Edgar Obare katika mawasiliano naye zinaonyesha kwamba mrembo huyo amekuwa akisumbuka fikra baada ya rafiki zake kumtumia links zinazoonyesha picha yake ikitumiwa katika ripoti za madai ya kuwa mpenzi mpya wa Willis Raburu .
Raburu na Marya wamekuwa na mwaka mgumu wa 2020 kwani baada ya kumpoteza mtoto wao kabla ya Marya kujifungua Januari tarehe moja, zimeibuka ripoti hizo kwamba wameachana .