Mjadala wa ugavi wa mapato unazua mgawnayiko hakuna kaunti inayofaa kuonewa-Ruto

Ruto
Ruto
Mjadala unaoendelea kuhusu mfumo wa ugavi wa mapato  kwa kaunti unazua mgawanyiko  ambao haufai ,amesema naibu wa rais William Ruto .

Ruto  amesema katiba inahitaji pawepo usawa katika ugavi wa raslimali  na kulitaka bunge kutekeleza jukumu lake  ipasavyo kwa kuhakikisha kwamba kila kaunti  inapata mgao inayohitaji .

" Bunge linafaa kuhakikishja kwamba mfumo unaotumiwa kugawa raslimali unaafikia ushindi kwa wote bila kuiumiza kaunti yoyote .Inawezekana’ alisema Ruto kupitia  Twitter .

Maseneta  wamekosa kuafikia mfumo unaofaa kutumiwa  kugawa paesa kwa serikali za kaunti . Utata huo umelemaza kupitishwa kwa mswada wa  wa  ugavai wa mapato .

Kabla ya mswada huo  kupitishwa kuwa sheria  na kusainiwa na rais Kenyatta hakuna kaunti itakayopewa fedha hizo .

Utata kuhusu mfumo unaotumiwa kwa ugavi wa pesa kw akaunti umezua mgawanyiko miongoni mwa vyama vya kisiasa huku ODM  ikionekana kutofautiana na upande wa jubilee unaomwunga mkono rais kenyatta unaotaka mfumo wa sasa uliopendekezwa kutumiwa .

Mwishoni mwa wiki  kiranja wa walio wengi katika senate  Irungu Kang'ata's alitishia kwamba hapatakuwa na BBI endapo  maseneta wa ODM hawataunga mkono mfumo huo unaopendekezwa na serikali .