Watu 15 wameaga dunia baada ya kutokea ajali mbaya kwenye barabara ya Mombasa kwenda Malindi katika eneo liitwalo Tororo .
Ajali hiyo ilitokea mwendo wa saa kumi na mbili jioni siku ya jumapili na ilihusisha Lori lililokuwa likienda Mombasa ambalo lilibadilisha mkondo kwa ghafla na kugongana ana kwa ana na matatu ya abiria .
Madreva wote ni miongoni mwa walioaga dunia papo hapo ilhali manusura watatu wapo katika hospitali ya wilaya ya kilifi wakiwa na majeraha mabaya . Kamanda wa polisi wa pwani Rashid Yakub amesema lori hilo halikuwa na mizgo wakati wa ajali .Miili ya waliofariki imepelekwa katika hifadhi ya maiti ya hospitali ya kilifi