Mkewe Bahati aungana na mashabiki kutuma rambirambi zao kwa msanii Weezdom

Aliyekuwa msajiliwa wa lebo ya EMB msanii Weezdom yuko katika maomboolezi hii ni baada ya kumpoteza rafiki wa karibu na mama lakini si mama mzazi ambaye aliaga dunia mnamo jumapili Agosti,30.

Kupitia kwenye mitandao ya kijamii Weezdom aliposti video huku akieleza jinsi mwendazake Faith Peter alimlea kama mama mzazi.

"Wacha ni seme kuwa zawadi ya maana humu nchini ni uhai, nimepata habari tu saa hii, kuwa nimempoteza mmoja wa watu wa maana katika maisha yangu na ambaye ningetamaini angekaa duniani ili atazame na kuona mafanikio yangu lakini nimempoteza hii leo

Rafiki wa karibu ambaye alikuwa familia kwangu ambaye wakati wangu mgumu alinishika mkono kama mama mzazi lala salama faith peter

https://www.instagram.com/p/CEhXGN5pqpL/

Rafiki ambaye alikuwa familia, lala salama mamaa 💔💔💔 utahishi kwa moyo wangu milele." Alisema Weezdom.

Pia aliposti picha ambazo walipigwa kabla ya kifo chake, inaashiria ya kwamba mwendazake amekuwa na Weezdom hapa na pale.

Mashabiki na mkewe Bahati walichukua fursa hiyo na kutuma risala za rambirambi kwa msanii huyo na hizi hapa baadhi ya jumbe zao;

diana marua: Pole Sana Weez! It will be well. May She Rest In Power ❤️🙏

🙏🙏🙏🙏 Take heart. Our prayers go to your family

: Woiye! Saddened. She had such a kind beautiful soul Woiye!!! RIP Faith. Pole Weez. I know how much you guys cared for each other. 💔💔💔💔

May the Lord comfort you family🙏 Poleni sana

My deepest condolences Weez🙏🏾 Rest well Mama🙏🏾🙏🏾:

:May She Rest In Peace🙏🏽

Rest easy beautiful🤗❤️❤️

guardianangelglobal: pole sana kaka