Mkewe Harmonize , Sarah amuandikia barua siku chache baada ya kumblock

Harmonize  na mkewe  wife Sarah Michelotti wameanza kuzua  mhemko sasa. Siku chache baada ya kila mmoja kukataa kumfuata mwenzake katika mitandao ya kijamii, Sarah amemuandikia Hamornize barua

Kipusa huyo raia wa  Italia  aliamua kuchukua hatua ya kuandika barua hiyo ili kuthibitisha kwamba yeye na msanii huyo bado wapo katika ndoa. Kumekuwa na uvumi kwamba huenda Harmonize na kipenzi chake wametengana lakini Michelotti  ametumia instagram  kuwafedhehesha mahaters  kwa kuiweka picha yake na Harmonize

Katika picha hiyo  Sarah alieleza jinsi anavyothamini mume wake akiandika;

 “The most expensive husband of my love.  Always on point baby,”

Hii ni baada ya kulipuka madai kwamba Harmonize  alimsaliti mkewe kwa kushiriki mapenzi na  Nicole Berry aliyehusishwa katika video ya wimbo wa bedroom wa msanii huyo. Wiki iliyopita, imesambaza video mtandaoni inayoonyesha mwanamke anayedaiwa kuwa Sarah akifoka makali nje ya nyumba inayodaiwa kuwa ya   Nicole Berry.  Pia kumekuwa na madai kwamba  Hamornize amekuwa akiishi na mwanadada huyo   jambo ambalo lilimpa hamaki Sarah .

Sarah bado hamfuati  Harmonize  katika instagram lakini alimtag katika posti yake ya mapenzi. Hatua ya Sarah na Harmonize  kuacha kumfuta kila mmoja katika insta ilizua hofu kwamba huenda ndoa yao ilikuwa imevunjika .