Mkusanyiko wa habari na Matukio muhimu Alhamisi 06.Juni. 2019

  Mlaghai akamatwa Gilgil baada ya kupokea  Sh.750,000 ili kuwaingiza vijana KDF

 Polisi huko Gilgil  wamemkamata mwanamme mmoja aliyemlaghai mwakamke shilingi elfu 720  kwa ahadi ya kumsaidia kuwaingiza wanawe wawili katika jeshi . Mshukiwa aliyejifanywa kuwa kapteini katika KDF alikamatwa katika chumba cha hoteli moja akingoja kupokea pesa zaidi . Polisi walifaulu kunasa barua feki za usajili  kutoka kwa mshukiwa huyo  huku wakigundua kwamba huenda waathiriwa zaidi walipunjwa fedha na mshukiwa huyo .

 

Mtu mmoja afariki kwa kugongwa na Treni  Changamwe

 Mwanamme mmoja ameaga dunia baada ya kugongwa na treni ya kubeba mizigo katika  eneo la bikirani  huko changamwe . mwathiriwa alikuwa akivuka   njia ya reli wakati alipogongwa  mapema leo .wakaazi sasa wanalitaka shirika la reli kujenda kivukio cha kuviunganisha vijiji vya  kwa punda na  Bikirani .

James Mburu  ateuliwa kuwa kamishna mkuu mpya wa KRA .

  Waziri wa fedha Henry Rotich  ametangaza uteuzi wa james mburu kama kamishna mkuu wa halmashauri ya KRA . Mburu atahudumu kwa kipindi cha miaka mitatu kuanzia julai mois mwaka huu .kwa sasa anahudumu kama  kamishna wa KRA kuhusu  uchunguzi na oparesheni maalum

 Juhudi za kuwaokoa Waliozikwa  na udongo wa shimo la choo Nyeri  zaendelea .

   Shughuli ya kuwatafuta watu watatu waliozikwa hao katika shimo la choo huko nyeri inaendelea .  kamanda wa polisi  Adiel Nyange amesema shughuli hiyo imeanza saa mbili asubuhi leo na wana matumaini ya kuwapata hai licha ya  juhudi za kuwaokoa kuchukua saa 24 .

  Sonko  afutilia mbali  kandarasi ya ununuzi wa magari ya City Hall

  Gavana wa Mike Sonko amefutilia mbali kandarasi ya shilingi milioni 400 ya ununuzi wa magari ya maafisa wakuu wa City hall .sonko amesema fedha hizo zitatumiwa kununua magari ya ambulansi  na ujenzi wa barabara .

   Filamu ya Rafiki itachezwa Kortini kama ushahidi

 Filamu yenye utata kwa jina rafiki itachezwa  kortini kama ushahidi katika kesi iliyowasilishwa na  mwelekezi wake wanuri kahiu . Korti imesema kuicheza filamu hiyo mahakama haitachelewesha kusikizwa kwa kesi hiyo kama  lilivyodai shirika la filamu nchini .