Mahakama moja ya Muranga imeamuru kwamba mwanandoa hafai kupata nusu ya mali moja kwa moja wakati wanapotalakiana . Jaji Kanyi Kimondo amesema kugawana mali kunafaa kutegemea mchango wa kila mwanandoa .Amesema pia kila mtu anafaa kuwa na ushahidi wa kuthibitisha mchango wake katika mali hiyo kabla ya kuiitisha kutoka kwa mwenzake .
Waaandamajai wakatiza usafiri mlolongo katika barabara kuu ya Nairobi –Mombasa
Usafiri umekatizwa leo katika barabara kuu ya Nairobi kwenda Mombasa huko mlolongo wakati waandamanaji walipoiziba kulalamikia ongezeko la visa vya uhalifu . Polisi wamekabiliana na waandamanaji hao kwa kuwarushia vitoa machozi na wamewashauri wenye magari kutumia njia mbadala .
Uvutaji ya shisha ni hatari kuliko hata sigara
Uvutaji wa shisha unaweza kudhuru mapafu yako haraka kuliko hata uvutaji wa sigara .Joel Gitali kutoka tobaco Alliance amesema vijana wengi wamekuwa wakivuta shisha wakifiri madhara yake sio mabaya kama sigara .
Acheni uhalifu ,Sonko awaonya vijana
Gavana wa Nairobi Mike Sonko amewahimiza vijana wanaojihusisha na uhalifu kukoma wovu huo na kuchukua hatua za kubadilisha mtindo wa maisha yao .Sonko amesema yuko tayari kuwasaidia vijana hao kujirekebisha ili kuepuka kuuwa na polisi .
Bilioni 7 kutumia kuzuia mafuriko Budalang’o na Siaya – Ruto
Serikali itatumia shilingi bilioni 7 kujenga mitaro na kuweka vizuizi vya kukabiliana na mafurko huko Budalangi na Siaya .Naibu wa Rais William Ruto amesema ukuta thabiti na mrefu utajengwa katika maeneo hayo ili kuthibiti maji ya mvua .
Wanakandarasi wataka kulipwa na Gavana Waiguru
Zaidi ya wanakandarasi 100 huko kirinyaga wamempa gavana Anne Waiguru makataa ya siku 30 kuwalipa deni lao la shilingi zaidi ya milioni 400 . Fedha hizo ni malimbikizi ya pesa za huduma na bidhaa walizoipa kaunti hiyo tangu mwaka wa kifedha wa 2015-2916 .
Hakuna maji Mombasa na Kilifi
WAKAAZI wa Mombasa na kilifi watakosa huduma za maji baada ya umeme katika kituo kikuu cha maji kukatizwa kwa ajili ya kutolipwa kwa bili . kampuni ya maji ya mombasa imetoa ilani hiyo kwa wakaazi baada ya wasambazi wa maji katika maeneo ya malindi na kilifi kukosa kulipa shilingi milioni 2 .
Polisi wanafaa kuongeza mishahara –Babi Owino
Mbunge wa Embakasi mashariki Babu Owino amependekeza mswada unaolenga kuwaongeza polisi mishahara .Mswada huo unalenga kuishurutisha tume ya kitaifa ya polisi kuwalipa polisi kulingana na kazi wanayofanya
Tutatekeleza vyema kazi ya kuunda sare za polisi –NYS
Shirika la NYS limeapa kutekeleza ahadi yake ya kutengeza sare mpya za polisi .Kaimu mkurugenzi mkuu wa shirika hilo Matilda Sakwa amesema kufikia mwisho wa mwezi huu ,sare zaidi ya elfu 16 za polisi zitakuwa tayari
Hakuna kupunguza umri wa mtu kufanya mapenzi –Matiang’i
Pendekezo la kupunguza umri wa mtu kufanya mapenzi kama mtu mzima halitakubalika .waziri wa usalama wa ndani Fred matiangi amesema hatua hiyo itahatarisha maisha ya vijana wadogo
Wizara ya leba na KNBS kufanya utafiti wa sekta ya juakali
Wzara ya leba na shirika la takwimu nchini zitafanya utafiti wa kitaifa ili kuratibu ujuzi na uwezo wa sekta ya jua kali .Waziri wa leba Ukur Yattani amesema shughuli hiyo ya siku 40 itakayoanza jumatatu inalenga kutambua mahitaji ya uajiri na ukuaji wa taaluma katika sekta hiyo .