Kitambulisho kilichopotea kilitumiwa kuisajili kadi ya simu iliyotumika katika mauaji ya wakili wa IPOA Willie kimani na watu wengine wawili . Moses kariithi ambaye kitambulisho chake kilitumika kuisajili laini ya simu iliyotumika amefika kortini leo kueleza kwamba kitambulisho chake kilipotea mwaka wa 2016 . aliripoti kupotea kwa kitambulisho hicho katika kituo cha polisi cha mlolongo na kisha akpewa kingine katika kituo cha Huduma .
Via vya ghasia na vya watu kujiua au matukio ya kutamaushwa ni mazngira mabyo huenda yakachangia mtoto kujaribu kujiua . mwanasaikolojia Riziki Ahmed amesema watoto kupitia nykati ngumu na ni muhimu kwa wazazi kuunda uhusiano wa kuwawezesha kustahimili changamoto hizo .
Mahakama ya juu zaidi imetupilia mbali pingamizi ya bunge kuhusu maamlaka yake ya kutoa maoni ya ushauri katika kesi iliyowasilishwa na serikali za kaunti kuhusu ugavi wa mapato . korti hiyo imesema maelekezo kuhusu masuala yote yalioibuliwa yatatolewa jumatano wiki ijayo.
Bunge la kaunti ya nakuru limeukataa mswada wa punguza Mizigo ,na kufikisha tano kaunti ambazo zimeukataa mswada huo kufikia sasa .spika Joel Maina amesema miongoni mwa sababu za kuukataa mswada huo ni pendekezo la kuvunjilia mbali maeneo bunge hatua anayosema itavuuga ugatuzi .
Vijana wanajiingiza katika utumizi wa dawa za kulevya wakiwa na umri wa miaka 13 .ufichuzi huo umo katika ripoti iliyotolewa na shirika la nacada kwa wizara ya elimu inayoeleza utumizi wa mihadarai miongoni mwa watoto wa shule .
Rais Uhuru Kenyatta ametuma risala za rambi kwa familia ,jamaa na rafiki za mwanafalsafa na msomi Samuel Mbiti . Uhuru amemtaja Mbiti kama msomi mashuhuri ambaye amekuwa kielelezo kwa wakenya wengi na alikuwa balozi muhimu sana wa Kenya katika mataifa ya nje .
Kamati ya senate kuhusu uhasibu imezidisha muda wa waranti ya kukamatwa kwa gavana wa machakos Alfred Mutua kwa wiki mbili baada ya gavana huyo kukosa kuwasili mbele ya kamati hiyo kwa mara ya pili leo . mwenyekiti wa kamati hiyo moses kajwang amesema hatua hiyo ya mutual ni kukaidi maamlaka ya bunge na pia ni ukiukaji wa sheria .