Rais Uhuru Kenyatta amefaulu kuafikia makubaliano na benki kuhusu mbinu bora za kuwapa vijana mikopo nafuu, almaarufu Stawi. Baada ya mashauriano na Rais, benki sasa zitaanza kutoa mikopo kwa riba ya asilimia 9 kwa vijana ili kuwasaidia kuanzisha shughuli za kujipa mapato.
Hazuna ya kitaifa kutoa pesa inazodaiwa kufikia mwisho wa mwezi
Hazina ya kitaifa itatoa shilingi bilioni 65 inazodaiwa kufikia mwisho wa mwezi huu . hilo limetangazwa leo wakati wa mkutano kati ya magavana na naibu wa rais william Ruto .
Maafisa wa usalama hawafai kuuawa hivi-mtaalam wa usalama
Udhaifu wa kufanya mipango na mikakati ya kiusalama ndio hatua inayofaa kulaumiwa kwa mauaji ya maafisa wa polisi .mtaalam wa masuala ya usalama Byron Adera amesema matumizi yafaayo na habari za ujasusi na mwongozo mzuri wa maafisa wa usalama ni mambo yanayofaa kuboreshwa ili kuzuia mauaji ya polisi katika jitihada za kukabiliana na ugaidi .
Rais Uhuru Kenyatta kuwateua Makamishna wa NCIC
Makamishna wa tume ya kitaifa ya Uwiano na utangamano sasa watateuliwa na rais na kuidhinishwa na bunge . marekebisho ya sheria sasa yanawaondoa wenyeviti wa tume ya haki za binadamu ,tume ya jinsia na usawa na ile ya usimamizi wa haki kuhusishwa katika uteuzi huo .
IMLU yataka uchunguzi zaidi kuhusu kifo cha mfungwa Naivasha
Shirika la Independent medical LEGAL Unit linataka uchunguzi wa kina kufanywa ili kubaini kilicho sababisha kifo cha mfungwa mmoja katika gereza kuu la naivasha . Samuel gitahi anadaiwa kupigwa na maafisa wa gereza hilo tarehe 13 mwezi huu baadaye akaaga dunia .
Sakwa ateuliwa rasmi kuwa mkuu wa NYS
Matilda Sakwa amethibitishwa kuwa mkurugenzi mkuu wa shirika la NYS . Sakwa ameteuliwa na rais uhuru kenyatta kupitia arifa ya gazeti rasmi la serikali ya tarehe 30 mei mwaka huu .
Wasioweza kuona walalamikia muundo wa noti mpya
Watu wenye ulemavu wa kuona wamelalakimia muundo wa noti mpya zilizotolewa na benki kuu kwani hazina alama za kutosha kuwawezesha kuzitambua . wamesema itakuwa vigumu kwao kuzitofautisha noti hizo .
Mtalii aliyekamatwa kwa ubakaji aachiliwa huru
Mtalii mmoja wa raia wa ujerumani aliyeshtumiwa kwa kumbaka msichana mwenye umri wa miaka minane ameachiliwa na mahakama moja ya malindi baada ya kupatikana kwamba hana hatia . korti imesema kwamba upande wa mashtaka ulikosa kuthibitisha kwamba Karl Ottomon alitekeleza kosa hilo
Jowie anyimwa dhamana kwa mara ya pili
Mahakama kuu kwa mara ya pili imemnyima dhamana mshukiwa wa mauaji Joseph Irungu kwa jina jingine Jowie . Korti imekataa ombi la Jowie ikisema halina msingi wowote .
Utalipia huduma za visa kutumia noti za kale
Wakenya wanaolenga kusafiri kwenda marekani wameshauriwa kulipia visa zao au huduma zozote katika ubalozi wa amerika kutumia noti za kale .ubalozi wa amerika nchini umesema unatayarisha utaratibu wa kuzikubali noti mpya zilizozinduliw ana serikali mwanzoni mwa mwezi huu .
Mawingu ba baridi ndio hali itakayoshuhudiwa katika sehemu nyingi
Hali ya mawingu itashuhudiwa katika nyanda za juu za kati ikiwemo Nairobi katika siku tano zijazo . idara ya utabiri wa hali ya anga imesema mvua zitashuhudiwa katika maeneo ya ziwa victoria , magharibi ,kati na kusini mwa Rift valley . upepo mkali pia unatarajiwa katika nusu ya mashariki ya taifa na katika ukanda wa pwani .
Wahadhiri wa chuo cha matibabu cha Moi wagoma
Wahadhiri katika chuo cha mafunzo ya matibabu cha Moi wamegoma wakitaka kulipwa malimbikizi ya marupurupu ya huduma za kliniki . katibau mkuu wa muungano wao ISHAMEL Ayabei amesema usimamizi wa chuo kikuu umeshindwa kuonyesha kujitolea kulipa fedha hizo tangia januari mwaka wa 2017 . Wameapa kulemaza shughuli zote za masomo hadi walipwe marupurupu hayo .