Gavana wa Nandi Stephen Sang aachiliwa kwa dhamana ya shilingi milioni 1
Gavana wa Nandi Stephen Sang ameachiliwa kwa bondi ya shilingi milioni moja na mdhamini wa kiasi kama hicho au dhamana ya shilingi laki tano pesa taslimu .Sang amekanusha mashtaka ya uharibifu wa mali ,uchochezi na kutumia vibaya maamlaka yake . Gavana huyo alilala seli baada ya kukamatwa na maafisa wa DCI huko kapsabet na kupelekwa katika kituo cha Central mjini kisumu .
Nitazidi kuwa mkali katika misimamo yangu -Magoha
WAZIRI wa elimu George Magoha amewakosoa wale ambao huchukulia msimamo wake mkali kuhusu masuala kama ujeuri . ameapa kuendelea kuwa thabiti katika maamuzi yake kuhusu masuala ya elimu .
Mwanamke ahukumiwa maisha jela kwa kumwua 'mpango wa kando ' wa mumewe
Mahakama moja huko Naivasha imemhukumu mwanamme mmoja mwenye umri wa miaka 36 kifungo cha maisha jela kwa kumwua mwanamke mwingine aliyekuwa na uhusiano wa kimapenzi na mume wake miaka mitano iliyopita .Cecilia Waruguru Muriithi alipatikana na hatia ya kumwua mwanafunzi wa sheria mwenye umri wa miaka 22 juni mwaka wa 2013 baada ya kugundua kwamba alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mumewe .
Chebukati asema IEBC iko tayari kushughulikia udhaifu wake
Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi na mipaka wafula chebukati anaamini kwamba tume yake itaweza kurekebisha makosa yalitokea wakti wa uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2017 . amesema wako tayari kushughulikia changamoto zote za kimpangilio na kisheria watakazokumbana nazo .
Watoto 3 wa Marehemu Kenneth Matiba wataka kulipwa fidia ya baba yao
Watoto watatu wa marehemu Kenneth matiba wanaitaka mahakama kuwapa idhini ya kuitisha malipo na kusimamia shilingi milioni 504 zilizopewa baba yao . Wanataka kufuatilia malipo ya fidia hiyo na kuhakikisha kwamba usimamizi wa mali yake hauathiriwi . pesa hizo ni fidia ambayo Matiba alipewa na mahakama kwa kukamatwa na serikali ya KANU alipokuwa akipigania siasa za vyama vingi .
Mwendesha mashtaka mfisadi Kitale apigw afaini ya shilingi 200,000
Mwendesha mmoja wa mashtaka katika afisi ya DPP huko kitale amepigwa faini ya shilingi laki mbili kwa kuitisha na kupokea hongo ya shilingi elfu 60 . amepatwa na kosa la kuitisha rushwa kutoka kwa mlalamishi ili kukataa ombi la mshukiwa kupewa dhamana katika kesi ya uhalifu mwaka wa 2014.
Mtoto wa miaka kumi amwua mwenzake Homabay
Mwanafunzi wa darasa la pili katika shule moja ya msingi huko homabay amemwua mwenzake baada ya kumsukuma walipokuwa wakicheza . Watoto hao walikuwa wakicheza hapo jana wakati mmoja alipomzukuma mwenzake ukutani na kumjeruhi .baadaye mtoto huyo alifariki alipokuwa akitibiwa katika kituo cha afya cha seka .
CBK yataka kanuni zake kufuatwa katika kubadilisha noti za kale
Benki kuu imewaonya maafisa wakuu watendaji wa taasisi za kifedha kuhakikisha kwamba mwongozo wake unatekelezwa kikamilifu kuhusu ubadilishanaji wa noti za zamani za shilingi 1000 ili kuzuia utakatishaji wa fedha . wanaotaka kubadilisha zaidi ya shilingi milioni moja za noti za kale wanahitaji kuwa na idhini maalum kutoka kwa CBK .
Mashahidi 33 kuwasilishwa dhidi ya Jackie Maribe na Joseph Irungu
Upande wa mashtaka umewatayarisha zaidi ya mashahidi 33 katika kesi dhidi ya mwanahabari Jackie maribe na Joseph Irungu walioshtakiwa kwa mauaji ya mfanyibiashara Monica Kimani .naibu mkurugenzi wa mashtaka ya umma catherine Mwaniki amesema wanne kati ya mashahidi hao 33 wamelindwa ilhali watano ni watalaam .kesi hiyo itaanza juni tarehe 25.
Mmoja afariki huku wanafunzi 2 wakijeruhiwa katika ajali Bungoma
Mtu mmoja ameaga dunia ilhali wanafunzi wawili wamejeruhiwa vibaya katika ajali ya barabarani huko bungoma. Ajali hiyo ilitokea kwenye barabara ya malaba kwenda kanduyi wakati gari dogo walimkuwa wakisafiria kupoteza mwelekeo na kugonga trela .
Kaunti zinafaa kukoma kukopa fedha
Tunahitaji kukomesha mtindo wa kukopa fedha na kuangazia njia mbadala za kutafuta mapato .mtaalam wa ugatuzi Mutakha Kangu amesema tunahitaji kutumia raslimali za kaunti ili kutafuta mapato zaidi .
Mwanafunzi wa JKUAT ajeruhiwa na polisi akijaribu kuingia Ikulu
Brian Kibet Bera, mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Kilimo na Teknolojia cha Jomo Kenyatta (JKUAT) mwenye umri wa miaka 25 jana alikamatwa na polisi kwa kuingia Ikulu ya Nairobi kinyume cha sheria.
Mwanafunzi huyo, ambaye alikwea lango moja la Ikulu, alipigwa risasi na kuumia katika bega la kushoto na maafisa wa polisi wanaopiga doria kwenye lango hilo baada ya kuchomoa kisu alipoagizwa asimame.
Uchunguzi unaendelea kufafanua nia yake ya kuingia Ikulu kinyume cha sheria na hatua zifaazo zitachukuliwa baada ya uchunguzi kukamilika.
Kenya yafunga mpaka wake na Somalia huko Lamu
Kenya imefunga mipaka yake na Somalia huko Lamu kwa muda usiojulikana huku oparesheni ya kudumisha usalama ikiendelea . Wakaazi wa vijiji vilivyoko kwenye eneo hilo pia wamepigwa marufuku kufanya bishara kupitia mpakani
Shule ya Sukwo huko Trans nzoia yafungwa baada ya vyoo kuporomoka
Shule ya msingi ya Sukwo huko Trans Nzoia imefungwa kwa muda baada ya mvua kubwa kusababisha vyoo 16 shuleni humo kuporomoka. Mwenyekiti wa muungano wa walimu na wazazi David Kimam anasema wamefunga shule hiyo kutokana na hofu ya mkurupuko ya maradhi.