Mnataka Simba aende nchi gani sasa? Swali la Ravanny baada ya Diamond kumtema Tanasha

Aisifuye mvua imemnyea, kilicho tarayajiwa kifanyike kishaa fanyika baada ya Tanasha kutengana na Diamond Platinamz, hali ilikuwa si hali tena wakati Diamond almzuia Tanasha kuondoka na mtoto wake siku ya Jumapili.

Msukosuko wa uhusiano wao ulianza pale msanii Simba alitoa wimbo wa jeje na mwanamke mwenye urembo wa kupindukia.

Kupitia mtandao wa kijamii, msanii Rayvanny aliwauliza mashabiki wake wanataka Simba awe na uhusiano wa kimapenzi na mwanamke wa nchi gani

Aliwashukuru wanawake ambao wana watoto wa Simba, msanii Simba ana watoto tofauti na wanawake tofauti wa nchi tatu za afrika mashariki.

Aliandika ujumbe huo baada ya mwenzake Diamond na mpenzi wake Tanasha kuachana.

"   Asanteni kwa watoto😂😂😂 tumemalizana na east africa,😂 mnataka simba asongee nchi gani tena? Rayvanny Aliandika.

Diamond anajulikana sana kwa kuwazalisha wanawake na kuachana nao hii ni kwa sababu ana macho ya mapenzi kila mahali anapoenda.

Alizidi kuandika kuwa kuna nchi ambazo Diamond almaarufu Simba hajaweza kuziguza, kutengana kwa Diamond na Tanasha kunajiri tu mwaka mmoja baada ya Rayvanny kukosana na mkewe

Ni post ambayo iliwafanya wengi wachangamke na kupeana hisia zao

yung_ahmed Jaribu wakamba uone kama hautageuka nyoka😂😂…na unajiita simba

joyous_86 What’s so funny about this break up🙄🙄🙄 did they have to remind us smh

chiwa5628 Father of all nations 😝😝😝😝😝😝😝

bridgetnajjuma I swear this is not funny how could they play with women’s feelings like this so stupid