Mono:Bintiye William Ruto ,Abby Cherop ajiunga na kidato cha kwanza Alliance Girls

Abby.jfif
Abby.jfif
Abby Cherop  ,bintiye naibu wa rais William Ruto aliyezaliwa katika uhusiano wa  pembeni  amejiunga na kidato cha kwanza katika shule ya wasichana ya  Alliance baada ya kupita mtihani wake wa KCPE kwa kupata alama 406 mwaka jana .

Katika picha zilizowekwa kwenye mitandao ya  kijamii  Abby alipelekwa shuleni  na mamake Priscah Jemutai Bett, pamoja na  jamaa zakekadhaa  na walionekana katika kituo cha mabasi  akiwa na   bidhaa zake wa kwenda shule . Bintiye Ruto aliangaziwa kwa mara ya kwanza mwaka wa 2017  baada ya mamake Bett  kumshtaki naibu w arias akitaka usaidizi wa kumlea  .

Ruto alijitokeza na kukiri kwamba Abby alikuwa mwanawe na alikuwa akitunzwa vizuri kinyume na madai ya mamake . Wawili hao walikutana  mwaka wa 2005 wakati  Bett alipokuwa mwanafunzi katika chuo kikuu cha  Moi  na Abby akazaliwa mwaka wa 2006 .