Mr Nice azungumza kuhusu kutiliwa sumu na alivyonusurika kifo

Miaka 7 iliyopita  mwanamuziki  Lucas Mkenda  alikimbizw akatika hospitali huko shinyanga Tanzania baada ya kuwekewa sumu .

Baadaye aliwalaumu watu aliosema walimuonea wivu kwa kupewa kazi  ya kuwafantia kampeini   wanasiasa fulani .

Akizungumza na Maina kageni katika kipindi chake cha asubuhi  ,Mr Nice amesema tukio hilo lilimshtua sana  na hakulizungumzia kwa muda mrefu ili kuhakikisha kwamba kwanza yuko salama .

Alisema waliotaka kumuua waliomuonea wivu kwa sababu ya mafanikio yake .

Alisema hivi kupitia mitandao ya kijamii

 ‘ kampeini za kisiasa i jambo la kupita na maisha huendelea baada ya  uchaguzi ,ni jambo baya kwamba mrengo wangu wa kisiasa ulinifikisha hospitalini

Akizungumza kuhusu hai yake ya kisasa ya kifedha Mr Nice alisema

“ tangu agostri mwaka jana nimekuwa napiga tours za muziki tanzania . pia nimeenda  sudan kusini ,rwanda na burundi kabla ya janga la corona kuwa tatizo na kunifanya nifutilie mbali ziara hizo .

Mr Nice  pia amejitetea kisema kwamba hatua yake ya kudidimia kimuziki haina uhusiano na uraibu wake wa kunywa pombe .

 “ sijawahi kuwa na tatizo la kunywa pombe  kupindukia  ingawaje mimi hunywa ,hilo halijawahi kuvuruga taaluma yangu katika muziki

Akijibu madai kwamba hana nidhamu Mr Nice amesema

 “ aliyetoa madai hayo lazima alinifanyia jambo ili kunifanya niwe hivyo