Msilete ghasia katika BBI-Ruto atoa rai baada ya vurugu za Kitui

Naibu wa rais William Ruto  amekashifu ghasia zilizoshuhudiwa siku ya jumamosi wakati wa mkutano wa BBI huko Kitui . Ruto amesema  hakuna utangamano na umoja unaoweza kuafikiwa kutumia ghasia  akisema kila mkenya ana hakika ya kusikizwa . “ sasa sio wakati wa kujigamba ,kupiga kifua na kuchukua misimamo mikali’ amesema Ruto katika shule ya wasichana ya Itoerio huko Kisii ." tufanye kazi kwa pamoja na tuvimiliane  ili tuweze kusikilizana . hata walio wanyonge wana jambo la kusema . mjadala huu  sio wa viongozi au wanasiasa pekee’ amesema Ruto.

Miongoni mwa viongozi waliomkaribisha Ruto na kuapa kumuunga mkono katika uchaguzi mkuu ujao ni pamoja na naibu gavana wa Kisii Joash Maangi ,wabunge Silvanus Osoro (South Mugirango)  na Alpha Miruka (Bomachoge Chache). Siku ya jumamosi kulikuwa na rabsha katika mkutano wa BBI huko Kituo ambapo baadhi ya washirika wa Naibu wa rais walihangaishwa na  watoa ulinzi pamoja na baadhi ya waliohudhuria mkutano huo.

Wabunge waliowasili baada ya mkutano huo kuanza walizuiwa kufika jukwani ambapo kiongozi wa ODM Raila Odinga alimywa ameketi  pamoja na kiongozi wa Wiper Kalonzo Musyoka ,magavana na viongozi wengine walioachaguliwa . Zaidi  watu 40 wa kutoa ulinzi waliwavizia na kuwazuia  viongozi wa tanga tanga wakiwemo  Kipchumba Murkomen  (Elgeyo Marakwet)  na  seneta wa Kericho Aaron Cheruiyot dhidi ya kufika jukwani . Moses Kuria pia aliyapitia masaibu kama hayo alipofurushwa kutoka mkutano huo .