Baadhi ya rafiki zake hawajafurahi baada ya kuachwa nje ya orodha ya wageni walioalikwa katika harusi hiyo . Lakini Bien hana cha kumpa wasia wasikwa sababu harusi ilikuwa yake na hakuna anayeweza kudai kuwa na haki ya kuhudhuria harusi ambayo hajapewa mualiko .
" Sina haja ya kuhudhuria harusi kwa sababu nimeenda katika harusi nyingi.Ilikuwa njia yangu ya kuadhimisha kujitolea kwangu kwa mke wangu’ amesema Bien .
Bien amewashauri wanaopanga kufanya harusi kuhakikisha kwamba wanaanda hafla wanazoweza kugharamia kwa urahisi ."Harusi ni mwanzo wa maisha yako .kwa hivyo usitumie pesa zakozote kufanya harusi .Fanya kitu unachoweza kugharamia .Hakikisha unatumia pesa nyingi katika fungate yako kuliko unazotumia katika harusi yako’ amesema Bien . Bien alitumia kiasi kisichozidi shilingi laki tatu katika harusi yake .Bien na Mke wake hawajaenda honeymoon kwa sababu ya mkurupuko wa virusivya Corona