Wakizungumza katika mji wa Sankuri siku ya jumatatu wakati wa ziara ya maendeleo, viongozi hao walisema kuwa wamepitia mapendekezo hayo ya Punguza mzigo na wamegundua kuwa mswada huo haujashughulikia maswala yanayoathiri watu katika kaunti hiyo ya Garissa.
Gavana huyo aliwasihi wanasiasa na wakaazi waepuke siasa za mapema na badala yake walenge nguvu zao kwa kuzidisha maendeleo.
Mbunge wa Balambala Omar Shurie alisema kuwa hakuna kitu chochote kizuri katika mswada unaopendekezwa na Ekuru Aukot wa chama cha Thirdway alliance.
Shurie aliwataka wajumbe katika bunge la kaunti hiyo ya Garissa kutupilia mbali mswada huo pindi tu utakapowasilishwa bungeni.
Mwezi uliopita, wajumbe wengi wakiongozwa na kiongozi wa wengi Mohamed Gabow na spika katika bunge hilo Ibrahim Abass waliahidi kuwa watapitisha mswada huo.
Wawili hao walihutubia waandishi wa habari baada ya kumsikiliza Ekuru Aukot akielezea maelezo yake.
Kwa sasa kaunti 14 yamekataa kupitisha mswada wa Punguza mzigo kwa msingi kuwa inalenga kupunguza idadi ya wawakilishi.