Mudavadi ataka mikutano yote ya kisiasa kupigwa marufuku

Mudavadi 2
Mudavadi 2
Wizara za usalama wa ndani na afya zinafaa kupiga marufuku  mikutano yote ya kisiasa  ili kuzuia kusambaa kwa virusi vya corona .

Mudavadi  amesema mikutano hiyo inahatarisha maisha ya wakenya hasa katika maeneo ya mashambani  ambao wanahudhuria mikutano hiyo .

Wanasiasa wakiwemo maafisa wakuu wa serikali na  mawaziri  wamekuwa  wakifanya mikutano na wananchi huku wakikosa kutii kanuni za wizara ya afya kuhusu kuzuia usmbaaji wa virusi vya corona .

Mudavadi amesema mikuano hiyo inawatia wakenya wengi hatarini.

“ virusi hivi ni hatari na tunafaa kuwa na tahadhari  ili kuwalinda watu wetu  kwa sababu wengi huenda wakaambukizwa virusi hivi’ amesema  Mudavadi .

Mudavadi  amesema eneo la magharibi ndilo linalowekwa katika hatari zaidi kwa sababu ya kuzidishwa kwa shughuli za kisiasa .  Ameongeza kwamba kanuni za wizara ya afya zimepuuzwa katika mikutano hiyo .

Mawaziri Peter Munya (Kilimo), James Macharia (Uchukuzi )  na  Eugene Wamalwa (ugatuzi )  wamezuru eneo hilo ili kuzuru miradi ya maendeleo  na kuwa wageni wa magavana wa kaunti za magharibi .Mudavadi  amesema wenyeji wengi wamekuwa wakihudhuria mikutano hiyo bila kuzingatia masharti hayo yaliyowekwa .