Mudavadi kuzuru eneo la Mlima Kenya kujipigia debe kwa uchaguzi mkuu 2022

Mudavadi
Mudavadi
Kiongozi wa chama cha Amani National Congress Musalia Mudavadi anapanga kuzuru eneo la Mlima Kenya ili kukitangaza chama cghake na azma yake kuwania urais mwaka wa 2022 . Mudavadi aliwaalika takriban waakilishi 20 wa wadi kutoka Nyeri siku ya jumatano .

Waakilishi hao  walimhakikishia  kwamba wako tayari kumuunga mkono katika nia yake ya kuwa rais ili kumrithi rais Uhuru Kenyatta .

“ Amekuwa wakikutana na viongozi mbali mbali  na makundi tofauti kutoka Mlima Kenya katika kipindi cha mwezi mmoja uliopita  na sasa yuko tayari kwenda eneo hilo kujitangaza’ amesema msemaji wake  Kibisu Kabatesi.

Mudavadi  tayari amekutana na kiongozi wa chama cha Narc Kenya Martha Karua  na aliyekuwa mbunge wa Gatanga Peter Kenneth.

Mkutano na wawili hao mwezi mei mwaka huu pia ulihudhuriwa na  Slly Kosgey aliyehudumu kama mkuu wa utumishi wa umma chini ya utawala wa rais wa zamani Daniel Moi .

Baada ya kukutana na Mudavadi ,Karua aliashiria uwezekano wa kuunda muungano wa kisiasa kati ya Narc Kenya na ANC kwa uchaguzi mkuu wa 2022 .

Karua  amesema anaendelea kuzungumza na Mudavadi na viongozi wengine wenye maono kama yake kutenegeza muungano thabiti wa kisiasa kabla ya uchaguzi mkuu ujao .

Kabatesi  amesema Mudavadi  amekuwa akitayarisha safari zake kwenda eneo la Kati  wakati ambapo amekuwa akikutana na viongozi kutoka eneo hilo .