Luwi ambaye ni baba na pia muigizaji alimshukuru mpenzi wake kwa kutembea naye wakati huo alipokuwa anapitia magumu.
Amemshukuru kichuna huyo kwa kuendelea kuwa imara katika uhusiano wao licha ya kusoma taarifa potovu zilizokuwa zinamhusu.
Akiandika ujumbe huo, Luwi aliongezea picha ya mpenziwe huyo na ambapo maelfu ya mashabiki wanaomfuatilia walimpongeza kwa kuchukua hatua hiyo.
Wiki moja iliyopita, Jacque Naisenya ambaye ni mpenzi wa Luwi alilazimika kuingilia kati baada ya watu kuita Luwi kama jamaa anayependa wanawake.
Jacque alisema kuwa ataendelea kusimama na mpenziwe wakati wa mazuri na mabaya.
Aliongezea kuwa watu siku hizi wameanza kutumia mitandao ya kijamii vibaya na kuharibia wengine sifa zao.
Luwi alikashifiwa na mwanamke kwa kutaka kumlipisha alfu 150 kwa lungula.
Mwanamke huyo alisema kuwa alimwandikia ujumbe Luwi kupitia ukurasa wake wa Instagram akitaka washiriki mchezo usiokuwa na mwamuzi japo na alipotuma pesa hizo, jamaa akatokomea.