Mume wa Janet Mbugua aziweka wazi picha za mtoto wao wa pili

janetandhubbyeddie
janetandhubbyeddie
Mtangazaji maarufu Janet Mbugua alijifungua mtoto wa kiume, Mali, mwezi wa September na hatujapata fursa ya kuona uso wake tangu kuzaliwa.

Eddie Ndichu mumewe Janet, alipiga picha na wanao wawili wa kiume wakiwa katika hafla ya familia na kuziweka kwenye mitandao za kijamii.

Ni hakika Mali anafanana na mama yake kama shilingi kwa ya pili lakini kwa hakika macho ni ya baba yake.

Janet amekua akiwaweka wana wao mbali na mitandao za kijamii kama wanavyo fanya kina mama wengi ambao ni mastar hapa Kenya.

Mwaka uliopita, Sharon Mundia alikuwa amemueka mtoto wake mbali na mitandao ya kijamii kama tu vile Janet ila bwana yake akiziweka picha hizo wazi kwa umati.

Mtazame mtoto Mali: