'Mume wangu alinikosea heshima!' Mugizaji Nyce Wanjeri afichua kilicho watenganisha

Nyce Wanjeri and Massawe Japanni
Nyce Wanjeri and Massawe Japanni
Aliyekuwa muigizaji wa kipindi cha 'Auntie Boss', Nyce Wanjeri ameeleza kilicho watenganisha yeye na aliyekuwa bwanake Tito.

Akizungumza na mtangazaji, Massawe Japanni katika kitengo cha Ilikuwaje, siku ya Jumatatu, Wanjeri ambaye walitengana na mumewe wa miaka tisa mwezi wa Novemba mwaka uliopita, alisema kuwa alikuwa anakosewa heshima.

Hayo yalitofautiana na sababu alizopeana Tito baada ya kuandika kwa mtandao kuwa walitengana baada ya Nyce Wanjeri kupata mafanikio katika sanaa.

Tito alisema kuwa tangia Nyce afanikiwe, hakuwa anampa yeye wala familia yao mda wa kutosha.

Soma ujumbe wake.

 “Why am I using Facebook? My marriage is over. So painful I swear. I saw it coming though. Success causes absenteeism, lack of bonding and lack of family time. Why did I imagine we last forever? We are both artists. It’s not normal. It doesn’t work,”

Nyce alisema kuwa utata kwa ndoa yao ilianza pindi tu ilipotimia miaka saba na miaka miwili baadaye, alishindwa kuvumilia ukosefu wa heshima kwake na kwa ndoa yao.

"Kwa kweli tumeachana, kwa nini? Sitaiongelea kwa sasa kwa sababu am not yet ready to share the story. Na ni ukweli, vile alisema tumewachana ni ukweli tumewacha kwa hivyo naweza sema he is single!" Alisema Muigizaji huyo.

Soma mahojiano yake na Massawe Japanni.

Je ni mashindano kati ya ndoa iliweza kusababisha mwisho wa ndoa yenyu?

Kila ndoa ina utatizo wake na kila mtu ana ile kitu nyinyi huwa na problems nayo, sitaki kuiongelea sana ni competition kwa sababu huwa tunasema watu wawili wanaotumia blanketi moja, mambo mengi hufanyika.

Na pia kwa hii industry yenye tuko pia kuna disrespect, if mtu ameku disrespect leo kesho, kesho kutwa na hai change pia wewe kama mtu kuna  wakati itafika utachoka.

Na pia kuna vitu nyingi sana ukiangalia kivyako unaona either unanyanyaswa hapa na pia naambianga watu kuwa sio vizuri kuona watu wengine wana behave hivi unadhania yangu pia tuka behave hivi inaweza kuwa sawa.

Ilikuwaje ukasema potelea mbali baada ya miaka tisa ya ndoa?

Kwa hapo ni vitu kadhaa zenye nasema siko ready kwa saa hizi kuzitoa, lakini ni vitu zenye kama mwanamke singeweza, ya kwanza ni disrespect na zingine mingi.

Unajua watu wengi waliingilia hiyo kitu kulingana na vile iliwekwa. Wakasema ashafika, ashapata pesa, ashaenda Nigeria, ashakuwa success kitambo walikuwa pamoja saa hizi hawako juu ya hiyo success. Hapana hapana! 

Pesa kwangu mimi husema hivi; Pesa huja na inaisha. Material things are nothing ile kitu ya maana ni je kuna upendo? na pia kuna heshima?

Pata uhondo kamili.

&feature=youtu.be