'Mungu anayesababisha mwanamke "tasa" kuimba,' Kambua apeana sababu za kusifu

Leo ikiwa tarehe 9, Novemba mwaka wa 2019, msanii wa nyimbo za injili na mtangazaji, Kambua ana sababu zaidi ya milioni moja za kumsifu mungu wake.

Hii ni kwa sababu leo ndio siku anayoadhimisha kuzaliwa kwake!

Siku hii inajia takriban miezi miwili tu baada ya kujifungua mtoto wake wa kwanza, Nathaniel baada ya miaka nyingi ya kujaribu bila mafanikio.

Kupitia mtandao wake wa Instagram, badala ya kusherehekea siku ya kuzaliwa, Kambua alitumia fursa hiyo kumsifu mungu wake, mungu wa Rebecca, mungu wa Hannah na mungu wa Sarah ambaye alisubiri miongo na miongo kabla ya mungu kufungua tumbo lake na kumjalia isaac.

Alisimulia kuwa baada ya mungu kumjalia na mwana, aliamua kujipatia mda ili aweze kulea mwanawe akisema kuwa kazi yake kuu imekuwa kumpa mtoto huyo upendo, kumkumbatia na pia kumbusu kila mara.
Anasema upendo na miujiza wake mungu umempa kila namna na sababu ya kuimba!

Soma ujumbe wake Kambua wa kupendeza,
A Mummy. A whole mummy! Ain't God good? Also, it's my birthday 🎉 Aaaaalso, I have missed you all. But I took time to be fully present in the season God ushered me into. My current ministry is in changing diapers, warm snuggles, and wet kisses🥰🤱🏾. Ah! This. God. Is. Too. Much. Too much! God of Sarah, Hannah, Rebecca...Kambua. The God who opens wombs and causes the "barren" woman to sing! Covenant keeping God. In Him there are no limitations. 

I am grateful to know a God who does great things through weak, broken people.

My JOY is FULL, and my confidence in His goodness is rock solid. 

Happy birthday to me💃🏾💃🏾💃🏾

.

.

"The rain came down, the streams rose, and the winds blew and beat against that house; yet it did not fall, because it had its foundation on the rock"- Matt 7:25