Mungu ni mwema! Huenda mkamuona Jacque Maribe kwenye runinga karibuni

Binti Jacque Maribe alikataa usaidizi wa hakimu aliyejitolea kumsaidia arudi kufanya kazi kwenye televishini.

Jacque alipokuwa kortini na aliyekuwa mpenzi wake bwana Jowi, walipewa kiapo cha kutosoma habari kwenye runinga na kisha baadae Jacque akaamua kujiuzulu kutoka Citizen TV.

Baada ya kutoka kwenye runinga ya Citizen TV, binti huyu amekuwa akifanya kazi mwenyewe na kujitafutia riziki kupitia biashara mbalimbali.

Hata hivyo,ni kama vile, binti huyu atatokea kwenye runinga zetu kwani alikataa usaidizi wa hakimu waziwazi.