Kagwe amesema wanaokana kwamba ugonjwa huo haupo basi wanafaa kuungoja. Katika siku ambayo Kenya imesajili vifo vingi vya watu wengi kwa siku moja kwa ajili ya virusi hivyo -12 , Kagwe amesema sasa ni jukumu la kila mkenya kujitunza mwenyewe.
"... Itawachukua muda gani wafahamu kwamba ugonjwa huo upo, iwapo mtu anapinga hilo basi hakuna unachoweza kufanya'
Kenya leo imesajili idadi ya juu ya watu walioaga dunia kwa siku moja kutokana na ugonjwa wa corona baada ya watu 12 kuaga dunia.
Waziri wa afya Mutahi Kagwe amesema wote walioaga dunia ni kutoka Nairobi. Amesema watatu waliaga dunia wakiwa nyumbani ilhali waliosalia walifariki wakiwa hospitalini.
Kagwe ameongeza kwamba visa 189 vya ugonjwa huo vimeripotiwa nchini katika saa 24 zilizopita na kufikisha jumla ya visa hivyo nchini kuwa 10,294. Visa hivyo ni kutoka kwa sampuli 1,205 na kufikisha jumla ya sampuli zilizopimwa hadi sasa kuwa 216,242.
Kati ya visa hivyo vipya, 106 ni vya wanaume ilhali 83 ni wanawake.
Nairobi inaendelea kuwa kaunti inayoongoza kwa idadi ya visa vingi baada ya watu 147 kupatikana na virusi hivyo. Kaunti nyingine ni
Kiambu 20, Machakos 11, Kajiado 5 na Mombasa 2.Waziri Kagwe amesem sampuli nyingine zilizokusanywa leo hazijapimwa kwa sababu ya changamoto ya kielektroniki .