Mtoto mvulana mwenye umri wa miaka mitano aliyekuwa na kisa cha kwanza kilichothibitishwa cha ebola nchini Uganda ameaga dunia . Mtoto huyo alikuwa akipokea matibabu katika kituo cha matibabu ya ebola huko Kasese karibu na mpaka wa Uganda na Jamhuru ya Kidemokrasia ya Congo .
Shirika la afya duniani WHO jana lilithibitisha kwamba kisa cha kwanza cha ebola nchini Uganda Kilitokea DRC ambako mchipuko wa ugonjwa huo hatari umeripotiwa .
Familia ya mtoto huyo ilikuwa imesafiri hadi DRC kuhudhuria maazishi na kurejea Uganda tarehe 9 juni .Alipelekwa hospitali akiwa na daalili za virusi vya ebola