Mvulana  aliyekuwa na ebola Uganda afariki

ebola virus
ebola virus
Mtoto mvulana mwenye umri wa miaka mitano  aliyekuwa na kisa cha kwanza kilichothibitishwa cha ebola nchini Uganda ameaga dunia . Mtoto huyo alikuwa akipokea matibabu katika  kituo cha matibabu  ya ebola  huko Kasese karibu na mpaka wa Uganda na Jamhuru ya Kidemokrasia ya Congo .

Shirika la afya duniani WHO  jana lilithibitisha kwamba kisa cha kwanza cha ebola  nchini Uganda Kilitokea DRC  ambako mchipuko wa ugonjwa huo hatari umeripotiwa .

Familia ya mtoto huyo ilikuwa imesafiri  hadi DRC kuhudhuria maazishi na kurejea Uganda tarehe 9 juni .Alipelekwa hospitali akiwa na daalili za virusi vya ebola