Mohamed alipatikana ameuawa Mei tarehe 4 na mwili wake ukiwa barabarani eneo la Makina karibu na mahakama ya Kibera. Makachero wamemkata mshukiwa huyo baada ya kuitathmini kanda ya video yaa ya CCTV. Alikuwa akielekea nyumbani alfajiri baada ya kufanya kipindi cha usiku cha ‘ Ukumbi wa Kiislamu’
Picha hiyo ya video ilimuonyesha mvulana huyo mwenye umri wa miaka 14 akiwa pamoja na watu wengine wane wanaoshukiwa kuwa majambazi wanaohudumu katika mtaa huo wa mabanda. Polisi wanasema washukiwa hao walimshambulia marehemu akiwa anaenda nyumbani. Kundi hilo kisha lilimwibia kabla ya kumdunga kisu kifuani na kumuua papo hapo.
Mshukiwa mmoja alivamiwa na wananchi kabla ya kutoroka. Polisi wanaendelea kuwasaka washukiwa wengine watatu na mwanamke anayeaminika kuwapa hifadhi washukiwa hao. Polisi wamesema kwamba mshukiwa wa pili alikamatwa na ndiye aliyetambua majina ya wenzake. Marijan alikuwa mwanahabari aliyejituma na alikuwa nguzo muhimu kuanzisha kituo hicho cha redio mwaka wa 2006.