Mwakilishi wa wadi ya Witeithie Julius Taki katika kaunti ya Kiambu ambaye gari laki lenye picha ya naibu wa rais William Ruto akiwa amevalia sare ya kijeshi ameshtakiwa kwa kuendesha gari lilisilofaa kuwa barabarani .
Taki alifikishwa kortini jumanne na kukabiliwa na shtaka la kuhudumu gari lilisolokuwa na mikanda ya usalama . mashtaka mengine yalikuwa ,kuwabeba abiria wengi kupita kiasi na kuwa vioo vyenye rangi . Alikana mashtaka hayo na kuachiliwa kwa dhamana ya shilingi 20,000 pesa taslimu .
Hata hivyo uhuru wa Bwana Taki haukudumu kwani upande wa mashtaka uliwasilisha ombi kutoka DCI kumzuilia ili kukamilisha uchunguzi kuhusu alikotoa nembo za serikali zilizokuwa katika gari lake . upande wa mashtaka umeimbia korti kwamba polisi wanahitaji kufahamu zilikotolewa nembo hizo . mahakama ilikubali ombi lao na kesi hiyo itasikizwa Juni tarehe nne .