Denis Abuga alishtakiwa katika mahakama ya kibera mbele ya hakimu mkuu Abdul Lorot na alikanusha mashtaka dhidi yake .
Polisi wanasema Abuga alitekeleza kosa hilo julai tarehe 9 katika kaunti ndogo ya Dagoreti ,Nairobi .
Amedaiwa kufanya ngono na mlalamishi bila idhini yake ,hatua inayochukuliwa kuwa ubakaji . Pia alishtakiwa kwa kosa la pili kwa kufanya kitendo kisichofaa na mtu mzima kinyume na sheria ya kupambaa na dhulma za kimapenzi .
Mshukiwa alikuwa amempigia simu mlalamishi kwamba angemtembelea ili kwenda kuchukua vitu vyake alivyokuwa ameacha katika nyumba yake .Mlalamishi alikubali .Wakati Abuga alipofika , mlalamishi alimuacha sebuleni na kwenda chumba cha kulala lakini Abuga alimfuata na kisha kuketi kitandani .
Ripoti ya polisi inasema mshukiwa alitaka kuzungumza na mlalamishi ambaye aliuambia kwamba alikuwa akijitayarisha kwenda anakofanyia kazi . ni wakati huo ambapo Abuga alianza kutumia nguvu na kumshika kisha akamtupa kitandani ,kufunga mikono yake kwa kamba ya mkoba wake na kisha kumbaka .
Aliwapigia simu majirani ambao walimpeleka hospitalini na kisha baadaye wakaripoti tukio hilo katika kituo cha polisi cha Kilimani .
Hakimu aliagiza kwamba mtuhumiwa alipe dhamana ya shilingi laki mbili na mdhamani wa kiasi kama hicho na kumuagiza afike katika kituo cha polisi cha Kilimani ili sampuli yake ia DNA ichukuliwe