Mwanafunzi Wa Kidato Cha Tatu Ateketea Baada Ya Bweni Kushika Moto Bondo

Mwanafunzi wa kidato cha 3 ameteketea kiasi cha kutotambulika  baada ya bweni la shule yao ya upili ya  Bar-kowino kaunti ndogo ya  Bondo kushika moto.

Mwanafunzi huyo aliyekua mgonjwa alikua amejipumzisha na wenzake wawili walioweza kuruka kutoka kwa dirisha wakati moto ulipotokea

Mwalimu mkuu wa shule hiyo John Mboga, anasema wanafunzi wengine waliokua madarasani kwa masomo ya usiku walifika kujaribu kusaidia lakini hawakuweza kwani moto ulikua tayari umesamba huku mwanafunzi huyo akiwa amekwama ndani.

Mkuu wa polisi mjini Bondo Paul Kiarie amethibtisha tuki hilo na kueleza kwamba uchunguzi umeanzishwa.

Naibu gavana wa Siaya Wilson Ouma Onyango amezuru shule hiyo na kutoa rambi rambi zake huku akishinikiza kuwepo kwa subra na utulivu.