Mwanamme mmoja anakukuza majeraha katika sehemu yake ya siri baada ya malumbano

Mwanamme mmoja mwenye umri wa miaka thelathini na moja kutoka kijiji cha Bwaro kata ya Lugusi kwenye kaunti ndogo ya Webuye mashariki anaendelea kukuza majeraha katika sehemu yake ya siri baada ya kuumwa na mpenziwe baada ya kuwepo malumbano.

Kulingana na mhudumu wa matibabu emmanuel mwanja wa zahanati ya bakisa mwanamme huyo alifika kwenye zahanati hiyo akiwa analia na kutibiwa japo akatumwa kwenye matibabu zaidi webuye.

Babake mwanamme huyo alisema kuwa mwanawe alikodesha shamba akidhani alitaka kutumia kujisaidai na ilishangaa kusikia kisa hicho.

Chifu wa kata hiyo Samwel nayombe alithibitisha kisa hicho na kuwashauri vijana kutumia mapato yao vyema. nao akina mama kutoka sehemu hiyo waliwashauri wanandoa kuwa waminifu ili kuepuka visa kama hivyo.

Brian O. Ojama