Kulingana na maafisa wa DCI, mwanaume huyo anayetambulika kama Justus Kamoja mwenye umri wa miaka 30, anatarajiwa kufikishwa mahakamani leo.
Katika kanda ya video hiyo, Kamoja anaonekana akimsukuma mlinzi huyo kwa fujo na kisha kufungua lako kuu na kutoka na gari lake.
Alifungua lango hilo kwa nguvu bila ruhusa kutoka kwa mlinzi wa mtaa.
Dhuluma hizo kutoka kwa Kamoja zimemtia mashakani na kwa sasa anatarajiwa kufikishwa mahakamani.
| Mr Justus KAMOJA who was captured on a video assaulting a female Security Guard at Komarock has been arrested. The 30yr old suspect will be arraigned in court once necessary Police action is complete. Many thanks to all those that contacted us! |
— DCI KENYA (@DCI_Kenya)
Afisi ya upelelezi wa makosa ya jina kupitia mtandao wa twitter umepongeza umma kwa kujitokeza na kukashifu tukio hilo.