Mwanaume kizuizini kwa kifo cha mkewe katika chumba cha kulala (lodge)

1048587_31
1048587_31
Ni vifo ambavyo vinatokea kila sehemu ya nchi visivyojulikana mwanzo wala mwisho na wala kilicho sababisha, ina maana wanadamu wamekuwa kama kuku wasiokuwa na hatia ya kuishi.

Mwanaume anaye tuhumiwa kwa kumuua mke katika chumba cha wageni cha kulala (lodge) ameweza kuzuiliwa kwa siku nane ili uchunguzi kufanyika kilicho sababisha kifo cha mwanamke huyo.

Emmanuel Owuor anatuhumiwa kwa kumuuwa Grace Adhiambo ambao waliweza kutengana katika ndoa yao na walikuwa wanajaribu kurudiana.

Polisi wa uchunguzi Joseph Wanjoi aliweza kueleza mahakama kuwa Owuor alilipa kadi kwa chumba kimoja katika hoteli moja ya GNK Hamza.

Katika barabara kuuu ya Jogoo Februari 7 kisha kumualika Adhiambo ili aweze kupatana na yeye katika hoteli hiyo.

Grace hakusuta mualiko huo aliweza kuenda bali hakutoka katika chumba hicho chenye walikuwa na Owuor, Mtuhumiwa anadaiwa aliweza kukimbia alipojua mke wake ameaga dunia.

Polisi walisema kuwa Owuor alishikwa na polisi Ijumaa.

Hakimu wa Makadara Heston Nyaga aliweza kumuuliza mtuhumiwa kama ana pingamizi kwa mashtaka au ombi hilo, kila mtu lazima ajitetee ata kama amefanya kosa aliweza kuomba aachiliwe.

"Naomba niachiliwe kwa maana naumia sana kwa ajili ya mke wangu amefariki, sikumuuwa mke wangu kwa sababu alikuwa na ugonjwa wa shinikizo la damu,

"Aliweza kuanguka chumbani," Alieleza Owuor.

Mtuhumiwa huyo ameweza kuwekwa katika rumande katika kituo cha polisi cha Buruburu, na kesi yake kutajwa Februari 22.

Grace Adhiambo ataweza kupata haki yake?

The Star/Carolyne Kubwa