OUT! Mwangi Kiunjuri aonyeshwa mlango katika mabadiliko serikalini .Orodha nzima ya walioteuliwa

Mwangi Kiunjuri  amefutwa kazi na rais Uhuru Kenyatta katika mabadiliko kwenye braza la mawaziri yaliyotangazwa jumanne . Kiunjuri alikuwa waziri wa Kilimo naye Adan alikuwa waziri  wa Jumuiya  ya afrika Mashariki .Raychel Omamo  amehamishwa hadi katika wizara ya  Mashauri ya kigeni   ilhali Sicily Kariuki  amehamishw ahadi katika wizara ya Maji . Peter Munya sasa ndiye waziri mpya wa Kilimo ilhali Monica Juma amehamishwa hadi katika wizara ya Ulinzi . Simon Chelegui amehamishwa kutoka wizara ya maji hadi ya leba ilhali  Ukur Yattani amethibitishwa kuwa waziri wa Fedha .

Aliyekuwa seneta wa Nyeri Mutahi Kagwe amerejea katika baraza la mawaziri kama waziri wa Afya  Naye Betty Maina ndiye waziri mpya wa Viwanda . Rais Pia amewateua makatibu wapya wa kudumu katika wizara  na  makatibu wa utawala katika wizara mbali mbalimbali kama ifuatavyo-John Weru  ameteuliwa kuwa katibu  wa kudumu wa  Wizara ya biashara ,Juan Ouma  ni katibu wa kudumu wa mafunzo ya anuwai , Mary Kimonye   ameteuliwa kuwa katibu wa kudumu wa Utumishi wa umma , balozi  Simon Nabukhwesi ameteuliwa kuwa katibu wa kudumu wa  elimu ya vyuo vikuu na utafiti , Solomon Kitungu ameteuliwa kuwa katibu wa kudumu wa Uchukuzi , Enock Momanyi Onyango ameteuliwa kuwa katibu wa kudumu wa Mipango ya  Majengo , Joe Okudo amehamishwa kuwa katibu wa kudumu wa Michezo ,Chris Kiptoo sasa ndiye katibu wa kudumu wa Mazingira , Kevit Desai  ndiye katibu wa kudumu wa jumuiya ya afrika mashariki ,Margaret Mwakima sasa ndiye katibu wa kudumu wa  ustawi wa maeneo ,Esther Koimett ndiye katibu wa kudumu wa  matangazo na mawasiliano,Peter Kaberia sasa ndiye katibu wa kudumu wa  madini , safina kwekwe  ndiye katibu wa kudumu wa Utalii  na Collete Suda ndiye katibu wa kudumu wa  Jinsia .

Rais Kenyatta pia amefanya uteuzi wa  makatibu wa utawala katika wizara mbali kama ifuatavyo-

Hussein Dhado –CAS   Wizara ya Usalama wa ndani

Patrick Ole Ntuntu- CAS Wizara ya Leba

Andrew Tuimur –CAS Wizara ya  maji

Abdul  Bahari –CAS Wizara  Ugatuzi na maeneo ya ASAL

Lawrence Karanja – CAS wizara ya  Viwanda na Biashara .

Peter Odoyo – CAS Wizara ya  Ulinzi

Maureen Magoma Mbaka- CAS Wizara ya  ICT na Ubunifu na masuala ya Vijana

Winnie Guchu – CAS Wizara ya  Sheria ya Serikali

Wavinya Ndeti – CAS Wizara ya Uchukuzi

Zachariah Mugure –CAS Wizara ya Elimu

Mumina Bonaya – CAS  Wizara ya Elimu

Lina Jebii Kilimo – CAS Wizara ya kilimo ,mifugo na Uvuvi

Ann Mukami Nyaga- CAS Wizara ya ya kilimo ,mifugo na Uvuvi

Mercy Mwangangi – CAS Wizara ya Afya

Nadia Ahmed Abdalla –CAS Wizara ya  ICT ,Ubunifu na masuala ya vijana .