Mwigizaji Nyce Wanjeri akana kuhusishwa na video ya ngono inayosambaa

Nyce Njeri
Nyce Njeri
Mwigizaji Nyce Wanjeri aliyejulikana kama Shiru katika kipindi cha Auntie Boss amewarai watumizi wa mitandao kutoanika hadharani wenzao mitandaoni.

Nyce hivi maajuzi amekuwa gumzo kutokana video ya ngono iliyodaiwa kuhusishwa naye na kusambazwa mtandaoni.

Hata hivyo, amekana madai hayo, huku akisema kuwa kidosho aliye kwenye video hiyo si yeye.

"Wale wanaonijua wanajua kwamba Nyce siyo kama huyo," Wanjeri alisema

Tuchukue kwa mfano iwapo huyo kidosho angekuwa mimi. Nimekuwa nikiwaambia hivi, watu hufanya mapenzi. Kila moja hufanya mapenzi. Lakini kwa hiyo video haikuwa mimi. Niamini, huwa siweki mambo ya maisha yangu hadharani. alifafanua.

"Hata kama ingekuwa mimi, isingekuwa hoja. Tatizo ni kuwa mbona watu wananiandama ? Wanawake tushikane mikono tukomeshe hizi dhuluma," alisema

Nyce alizungumza hayo katika hafla ya tuzo za Kalasha ambapo alituzwa kuwa mwigizaji bora wa drama za  filamu za runinga.