Mzozo wa Kidiplomasia wanukia baina ya Kenya na Tanzania

MAGUFLI
MAGUFLI
Siku moja baada ya Kenya kutoijumuisha Tanzania katika orodha za nchi ambazo ndege zake zitaruhusiwa kuingia nchini Kenya, tanzania imepiga marufuku ndege za shirika la Keonya Airways kuingia nchini humo.

katika barua kwa Kenya Aieays, mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya shughuli za ndege nchini Tanzania Hamza Johari alisema kwamba aliafika uamuzi kufutilia mbali idhini ya ya ndege za KQ kuingia nchini humo.

Alisema kwamba Tanzania ilikuwa imetamaushwa na hatua ya Kenya kuifungia nje ya nchi ambazo zinaruhusiwa nchini Kenya wakati safari za ndege za kimatifa zinaporejea nchini Kenya.

Johari alisema kwamba barua hii mpya inafuta maafikiano yote ya awali yaliokuwa yameipa KQ idhini kuingia nchini humo ikiwemo barua ya Julai 30, 2020.

Kuingana na waziri wa uchukuzi James Macharia nchi zilizopewa idhini kuingia Kenya ni Uchina, Korea Kusini, Japan, Canada, Zimbabwe na Ethiopia. Nchi zingine zilizoruhusiwa ni Ufaransa, Rwanda, Uganda, Namibia na Morroco.

waziri alisema nchi zilzoewa idhini zimesajili kupungua kwa maambukizi ya vrisi vya corona. lisema .orodha hiyo itafanyiwa mabadiliko kila mara kulingapna na hali itakavyokuwa na utathmini wa usambaaji wa mvirusi vya corona kote duniani.

Tanzania imelaumiwa kwa kuficha tawimu kuhusu maambukizi ya virusi vya corona. Mara ya mwisho nchi hiyo kutangaza deta za maambukizi ya covid-19 ilikuwa Aprili 29, ambapo jumla ya watu 480 walikuwa wameambukizwa na 21 wakifariki.

Siku ya Jumatatu rais Uhuru Kenyatta aliwatawahadharisha wakenya dhidi ya maeneo ambayo yamekataa kuwaeleza wananchi wake habai halisi kuhusu maabukizi ya corona.

“Tusijilinganishe na kusema kwamba baadhi ya maeneo hayana virusi. Mbona tuko nayo na wao hawana? Wacha niwakumbushe wakenya, tunaishi katika demokrasia, ambapo kuna uhuru wa vyombo vya habari. Kama taifa hatuna uwezo wa kuficha kitu chochote. Kinachofanyika tunawaambia,” Uhuru alisema.

Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli amekuwa akisema kwamba nchi yake tayari meshinda corona na kushauri wananchi wake kuenelea na shughuli zao bila tashwishi.