Aliyekuwa kapteni wa timu ya taifa ya soka Harambee Star Musa Otieno ameruhusiwa kwenda nyumbani kutka hospitalini .
Otieno amekuwa katika hospitali kuu ya KNH kwa siku 10 akipokea matibabu kwa maradhi yenye dalili kama za virusi vya corona. Nyota huyo wa zamani mwenye umri wa miaka 46 amemshukuru Mola na wote waliomtakia afueni ya haraka alipokuwa kitandani.
Amesema hali yake imeboreka lakini atalazimika kujitenga kwa siku 14 zaidi kama inavyotakikana na wizara ya afya.