Nairobi litakuwa jiji jipya kufikia Disemba asema Badi

badi
badi
Nairobi  itakuwa mji mpya kufikia Desemba mwaka huu, amesema mkurugezi mkuu wa NMS  Mohamed Badi.

Akizungumza na KTN,  Badi amesema kundi lake  limefaulu kuchimba visima 93 katika siku  100 zilizopita. Badi amesema  kupitia  mpango huo, maji yatakuwa yakipelekwa kwa wakaazi wa jiji bure bila malipo  katika mitaa ya mabanda.

Ameongeza kwamba   eneo la katikati mwa jiji linafanyiwa mageuzi  ndio kwa sababu kuna mrundiko wa taka kwa ajili kuna kazi zinazoendelea kutekelezwa kwa miezi 3 hadi 6 ijayo.

Ameongeza kwamba mamlaka hiyo hailengi kutwaa mipango ya gavana Sonko bali itaunganisha mipango hiyo ili itekelezwe kwa manufaa ya wakaazi wa Nairobi.

Badi amesema wana mpango wa kumaliza tatizo la uhaba wa maji jijini.

"Tumekuwa na makundi ambayo yanahujumu  juhudi za serikali ya kaunti kutoa huduma kama maji, umeme na miundo msingi. Sasa tupo katika harakati za kusajili  wauzaji wote wa maji  ili tujue wanayatoa wapi maji na wapi wanayasambaza’ amesema Badi.

Siku ya Jumatatu, Badi alisimamisha ujenzi wa  jumba moja la mstawishaji wa kibinafsi katika eneo la Parkland ambapo aliandamana na mwakilishi wadi wa eneo hilo  Jayendra Malde na mbunge wa Westlands Timothy Wanyonyi  na kipande hicho cha ardhi kilichokuwa kimenyakuliwa sasa kitatumiwa kujenga kituo cha afya kuwasaidia wenyeji.