'Najuta kuwafungulia wanangu akaunti za instagram,'Akothee

Ni mengi hufanywa na kusemwa na mwisho wake kuwa majuto, baada ya mwanahabari Lilian Muli kuposti ujumbe kuhusu wazazi ambao wamewafungulia wanao akaunti za instagram, mashabiki, na wasanii walitoa hisia tofaui huku msanii Akothee akijuta kwanini alifungulia watoto wake akaunti hizo.

Msanii Akothee anafahamika sana kwa ujasiri wake na hata moyo wenye utu, huu hapa ujumbe wake kuhusu majuto yake,

"Najuta kwanini nilifungulia watoto wangu akunti za instagram, sasa anataka nambari yake ya siri sasa anamiaka kumi na miwili, watu ambao wanamfuata kwenye mitandao hiyo hawafahamu

Wengine ni wabaya na wengine na wengine ni wa ukweli, niamini ni vibaya." Akothee alijibu ujumbe wake Lilian Muli.

(I am regreating why I opened accounts for my kids , now my son wants his password he is 12 now 😳😳😳 ,the people following him he doesn't know them,some are mean some are real ,trust me it's wrong 😳😳😳😳)

Je ni vyema kumfunguliwa mwanao akaunti za mitandao ya kijamii kama hajitimu umri huo?